Saturday, December 21, 2013

*SIMBA BILA OKWI & KASEJA INAWEZEKANA! YAICHAPA YANGA 3-1


 Kocha Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic, akiruka hewani kushangilia bao la kwanza la Simba lililofungwa na Hamis Tambwe katika dakika ya 14, ya kipindi cha kwanza.
 Mshambuliaji wa Simba Hamis Tambwe, akifunga bao la pili kwa mkwaju wa penati katika dakika ya 44, baada ya beki wa Yanga, David Luhende kumkwatua Ramadhan Singano katika eneo la hatari.
Mshambuliaji wa Yanga, Didier Kavumbagu, akijaribu kumfinya beki wa Simba, Joseph Owino wakati wa mtanange huo. Mpira sasa ni kipindi cha pili

Saturday, September 7, 2013

BOFYA HAPA NYIMBO MPYA YA DIAMOND-MY NUMBER 1

KUNANI JUSTIN BEIBER NA PARIS JACKSON

Baadhi ya watu wajiuliza ukaribu wao

*STARS YAWASILI BANJUL, KUIVAA GAMBIA LEO



Na Boniface Wambura, Banjul +2207362384
Kikosi cha Taifa Stars kimewasili salama hapa Banjul, Gambia tayari kwa mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya wenyeji itakayochezwa leo Septemba 7.

Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager imewasili hapa jana (Septemba 5 mwaka huu) saa 11 jioni ikitokea Dakar, Senegal ambapo ilichelewa kuunganisha ndege, hivyo kuamua kutumia usafiri wa barabara kwa vile ni karibu na baadaye kupanda kivuko kuingia Banjul badala ya kulala na kuchukua ndege nyingine siku inayofuata.

Wachezaji wako katika hali nzuri na leo jioni wanatarajia kufanya mazoezi ya mwisho kwenye Uwanja wa Independence ulioko Bakau ambao utatumika kwa mechi ya kesho. Timu imefikia hoteli ya Seaview iliyoko kandokando ya Bahari ya Atlantic.

Mechi hiyo itaanza saa 10.30 jioni kwa saa za hapa ambapo nyumbani Tanzania itakuwa saa 1.30 usiku, na itachezeshwa na waamuzi kutoka Rwanda Munyemana Hudu. Waamuzi wasaidizi ni Theogene Ndagijimana, Honore Simba na Issa Kagabo. Kamishna ni Andy Quamie kutoka Liberia.
Washabiki na vyombo vya habari vya hapa wanaizungumzia mechi hiyo ambayo ina umuhimu mkubwa kwa pande zote, huku Gambia ikiwa imeita wachezaji tisa wanaocheza barani Ulaya na Marekani. Gambia ambayo imepata uongozi mpya wa Chama cha Mpira wa Miguu Gambia (GFA) imepania kuhakikisha haimalizi mechi za mchujo ikiwa na pointi moja tu.

Kwa upande wa Tanzania, Kocha Kim Poulsen amesema nia ni kuona Stars yenye pointi sita inamaliza katika nafasi ya pili nyuma ya Ivory Coast ambayo tayari imechukua tiketi pekee ya kucheza raundi ya mwisho kutoka kundi hili la C.

“Mechi hii ni muhimu kwetu kwa vile tunataka matokeo mazuri ugenini. Lakini kikubwa ni kuwa matokeo mazuri si tu yatatuweka katika nafasi ya kuwa wa pili, lakini vilevile yatatusaidia kuongeza pointi kwenye viwango vya ubora vya FIFA, na kikubwa zaidi hii ni sehemu ya maandalizi ya sisi kucheza Fainali za Afrika za 2015,” amesema Kim.

Stars inatarajiwa kupangwa hivi; Juma Kaseja, Vincent Barnabas, Erasto Nyoni, Nadir Haroub, Henry Joseph, Frank Domayo, Haruni Chanongo, Amri Kiemba, Mrisho Ngasa, Simon Msuva na Khamis Mcha

*REDD'S MISS TANZANIA 2013 WATEMBELEA RADIO 5 YA JIJINI ARUSHA



Mtangazaji wa kipindi cha burudani cha Funika Base kutoka Radio 5 ya Mjini Arusha , Julius Kamafa (kushoto) akifanya mahojiano na Washiriki wa Shindano la Redd’s Miss Tanzania 2013 katika studio za redio hiyo jana.
 Baadhi ya warembo wakijieleza Live Redio 5 hii leo walipotebelea kituo hicho. KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPO CHINI

FIESTA KUWASHA MOTO MBEYA.



Msanii wa muziki wa kizazi kipya,ambaye kwa sasa anafanya vyema kwenye anga za muziki huo,Neylee akiimba kwa hisi jukwaani huu wakati tamasha la Serengeti Fiesta likiendelea kwa shangwe ndani ya uwanja wa Sokonine.
Wakazi wa jiji la Mbeya wakiwa wamejitokeza kwa wingi usiku huu kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2013 ndani ya uwanja wa Sokoine,ndio kwanza shoo inaanza ambapo msanii aliyewahi kuiwakilisa shindano la BSS,Walter Chilambo ndiye aliyefungua pazia la onesho hilo usiku huu. 

 Tamasha la Serengeti Fiesta 2013 likiendelea usiku huu kwenye uwanja wa Sokoine,Mkoani Mbeya
 Mama wa miduara ya Kibongofleva,Shilole akiwa na madensa wake wakitumbuiza jukwaani usiku huu ndani ya tamasha la Serengeti fiesta 2013,ndani ya uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya. KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPO CHINI

Friday, August 9, 2013

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL ASHIRIKI SWALA YA SIKUKUU YA IDDI KITAIFA MKOANI TABORA

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitoa salamu maalum za Sikukuu ya Iddi baada ya Swala iliyofanyika Kitaifa Mkoani Tabora katika Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi leo.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal (wa sita kutoka kulia), akishiriki na waumini wa dini ya Kiislamu katika Swala ya Sikukuu ya Iddi, iliyoswaliwa Kitaifa kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi Mkoani Tabora leo.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akijumuika na waumini wa dini ya Kiislamu katika Swala ya Sikukuu ya Iddi iliyoswaliwa Kitaifa kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi Mkoani Tabora leo.
 Sehemu ya Waumini wa dini ya Kiislamu waliojitokeza kuhudhuria Swala ya Sikukuu ya Iddi, iliyoswaliwa Kitaifa kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, Mkoani Tabora leo.
  Sehemu ya Waumini wa dini ya Kiislamu waliojitokeza kuhudhuria Swala ya Sikukuu ya Iddi, iliyoswaliwa Kitaifa kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, Mkoani Tabora leo.
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akijumuika na waumini wa dini ya Kiislamu katika Swala ya Sikukuu ya Iddi iliyoswaliwa Kitaifa kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi Mkoani Tabora leo.

  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akijumuika na waumini wa dini ya Kiislamu katika Swala ya Sikukuu ya Iddi iliyoswaliwa Kitaifa kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi Mkoani Tabora leo.


  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akijumuika na waumini wa dini ya Kiislamu katika Swala ya Sikukuu ya Iddi iliyoswaliwa Kitaifa kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi Mkoani Tabora leo.

Huyu Mzungu kwa ugali kama mmbongo

Cheki unga wake katika Ndoo, yaani Kiuswazi zaidi, Mzingira sasa yaani Ndo Kiuswazi Hasaaaa.!!!  Au ndo kusema Simba anapozidiwa...........

Sunday, July 7, 2013

*DKT SALMIN NA DKT SHEIN WAUNGURUMA KIBANDA MAITI ZANZIBAR LEO


 Makamu wa Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais Mstaafu wa  Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi (Komandoo) Dk.Salmin Amour Juma, alipokuwa akiwasalimia na kuwahutubia katika Mkutano wa hadhara

Kibandamaiti Mjini Zanzibar katika uwanja wa Demokrasia Kibanda maiti mjini Zanzibar.

Makamo wa Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akizungumza na wananchi na wanachama wa CCM wa Mikoa ya Unguja,katika Viwanja vya Demokrasia Kibanda maiti mjini Zanzibar,katika mkutano huo ulizungumzia uwepo wa Serikali mbili kwa Serikali ya mapinduzi Zanzibar na Serikali ya Muungano wa Tanzania.
Wanachama wa CCM wa maskani ya Kisonge wakishangilia katika Mkutano wa hadhara uliofanyika leo na kuhutubiwa na Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais wa Zanzibar  na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,Uwanja wa Kibandamaiti Mjini Zanzibar. Picha na Ramahan Othman,Ikulu.

*RAIS WA ZANZIBAR*RAIS WA ZANZIBAR ATEMBELEA MAONYESHO YA SABASABA ATEMBELEA MAONYESHO YA SABASABA


 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa  Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Kikundi cha ZAYDAT &BASMA GROUP cha Chukwani Zanzibar,TatuSuleiman,wakati alipokuwa  akiangalia bidhaa Mbali mbali za vikundi vya Ushirika kutoka Zanzibar vilivyoshiriki katika maonesho ya sabasaba ya kibiashara katika viwanja vya mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam jana.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa  Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa  Bana Enterprises Company Limited SAID OMAR SAID, kampuni ambayo inajishuhulisha na utengenezaji wa fanicha za Mti wa Mnazi,wakati alipotembelea maonesho ya sabasaba ya kibiashara katika viwanja vya
mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam jana.
  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa  Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Mke wa Rais Mstaafu Mama Anna Mkapa,wakati alipowasili katika Mabanda ya Taasisi yake (Mfuko wa Fursa sawa kwa Wote),alipotembelea maonesho ya sabasaba ya kibiashara yanayoendelea katikaviwanja vya mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa  Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,  akipata maelezo wakati alipokuwa
akiangalia Bidha mbali mbali za Akima mama kutoka Mkoani Kagera katika maonesho ya sabasaba ya kibiashara yanayoendelea katikaviwanja vya mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa  Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, akitoa ushauri kwa wasimamizi wa  kampuni ya Nguo ya Arusha chini ua usimamizi wa Mkurugenzi wake Anuj Shal,(kulia) wakati wa maonesho ya sabasaba ya kibiashara yanayoendelea katika viwanja vya mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam. Picha na Ramadhan Othman,Ikulu

*RAIS KIKWETE ANOGESHA TAMASHA LA MATUMAINI UWANJA WA TAIFA DAR


Rais kikwete akifungua tamasha la matumaini hivi sasa uwanja wa Taifa,jijini Dar.Picha zaidi zitawajia hapo baadae kidooogo.
Waimba injili Ambwene Mwasongwe (kulia) na Edson (kushoto) wakiimba sambamba katika Tamasha la Matumaini 2013.
Edson akishambulia.
Ambwene Mwasongwe naye alikuwepo.
Sehemu ya mashabiki wakishangilia burudani

*TAASISI LA STARKEY HEARING FOUNDATION YAWATIBU WALEMAVU WASIOSIKIA


 Nyota wa mchezo wa mpira wa miguu wa Marekani (American Football) Rays Lewis akimpa  Rais Dkt. Jakaya Kikwete zawadi ya kofia yenye nembo ya timu yake wakati nyota huyo alipomtembelea Rais Kikwete mjini Arusha. Nyota huyo yuko nchini ambapo ni mmoja wa wafadhili wakubwa wa huduma kwa wagonjwa wenye ulemavu wa kusikia inayotolewa na taasisi ya Starkey Hearing Foundation ya nchini Marekani.Wagonjwa zaidi ya 3500 wanatarajiwa kunufaika na huduma hiyo inayotolewa bure na taasisi hiyo.
 Muasisi wa Taasisi ya Strakey Hearing Foundation  Bwana Bill Austin Starkey akimhudumia mtoto Lissa Frank(9) ambaye alikuwa kiziwi tangu kuzaliwa na kuweza kusikia baada ya kupata tiba na huduma ya kuwekewa kifaa maalumu katika kliniki maalumu iliyofanyika katika hospitali ya Seliani mkoani Arusha leo.
Waasisi wa Taasisi ya Starkey Foundation Bwana Bill Austin Starkey(kulia aliyeinama) na Mkewe Tani Austin(Wapili kushoto) pamoja na mhudumu kutoka hospitali ya Seliani(kushoto) wakifurahi baada ya mtoto Lissa Frank(9) kuweza kusikia vyema baada ya kupatiwa matibabu katika kliniki maalumu iliyofanyika katika hospitali ya Seliani mjini Arusha leo. (Picha na Freddy Maro) 

BASI LA SUMRI LAUA TISA LAJERUHI 53 KATAVI.


Basi la kampuni ya Sumry limetumbukia mtoni na kusabisha watu tisa kupoteza maisha na kujeruhi abiria wapatao 53 katika mto Iku uliopo katika kijiji cha Sitalike wilaya ya Mlele mkoani Katavi
 Tukio hilo la kusikitisha lilitokea saa sita usiku kuamkia Julai 5, 2013 wakati basi hilo lilipokuwa likitokea mjini Sumbawanga kuelekea Mpanda mkoani Katavi likiwa na abiri waliokuwa wametoka Mbeya.
 Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Katavi Emanuely Nnley alisema  kuwa ajali hiyo ilihusisha basi aina ya Nissan Diesel lenye namba T909 AZT mali ya kampuni ya Sumry lililokuwa likiendesha na dereva aliyetajwa kwa jina na Stephano Chimane maarufu kwa jina la Ntungu.
  Mganga mkuu wa wilaya ya Mpanda Mkoani Katavi, Dr Emanuely Kamgobe alisema basi hilo lilipofika katika daraja hilo lenye kona kali na mteremko dereva wake alishindwa kulenga daraja hali iliyosababisha tairi za nyuma kupanda juu ya ukingo na kudumbukia mtoni ambapo dereva huyo alitoka  na kukimbilia kusikojulikana.
 Alifafanua kuwa juhudi za uokoaji zilianza kufanyika usiku huo huo ambapo majeruhi 53 waliokolewa na maiti tisa za wanaume watatu na wanawake watano na 
mtoto mmoja wa kike ziliopolewa katika maji 
 Alisema hali ya majeruhi inaendelea vizuri isipokuwa majeruhi watatu walikimbizwa katika hospitali ya mkoa wa Rukwa kwa matibabu zaidi na kufafanua kuwa chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa dereva kushindwa kuliongoza gari, ubovu wa gari na wembamba wa daraja 
 Afisa Mwandamizi wa SUMATRA mikoa ya Rukwa na Katavi, David Chiragi alisema basi hilo lilikuwa limeiba njia kwani leseni yake inaliruhusu basi hilo kufanya safari za Sumbawanga Kirando na siyo Sumbawanga Mpanda kwa mujibu wa leseni iliyotolewa mwezi Juni mwaka huu 
 Alisema hata upana wa daraja ilipotkea ajali hiyo ni mdogo sana ambapo vipimo vinaonesha daraja hilo lina upana wa mita 3.5 (tatu na nusu) tu wakati basi lina upana wa mita nne na nusu hivyo kujenga mazingira ya ugumu wa dereva kulenga daraja inapotokea msukosuko wa aina yoyote hasa wakati wa usiku na hivyo kuwataka wakala wa barabara mkoani Katavi kuangalia namna ya kupanua daraja hilo na kuboresha eneo hilo 
 Alisema katika kipindi cha Januari hadi July 2013 zaidi ya ajali tisa zimetokea katika daraja hilo zikihusisha magari makubwa saba na madogo mawili kutokana na madereva kushindwa kumudu magari yao na kulenga daraja hilo 
 Alisema pia basi hilo lina makosa ya kutembea nje ya ratiba, kuiba njia na kuzidisha abiria hivyo ofisi yake imechukua hatua ya kuvunja safari za mabasi ya kampuni ya Sumry za mchana na badala yake mabasi yote yataondoka Sumbawanga na Mpanda majira ya asubuhi pekee.

*NMB CHAPCHAP AKAUNTI YAWA KIVUTIO KIKUBWA KATIKA MAONYESHO YA SABASABA


 Maafisa Mauzo ya Nje wa Benki ya NMB wakiwahudumia wateja waliofika katika Banda la benki ya NMB lililopo katika viwanja vya sabasaba kwaajili ya kufungua akaunti ya Chapchap ambapo mteja ufunguliwa akaunti yake papo hapo na kupewa kadi ya kutolea pesa kwenye mashine muda huo huo.
 Baadhi ya Wateja waliofurika katika moja ya gazebo la NMB lililopo nje ya Banda la Benki ya NMB  katika Viwanja Vya Sabasaba wakifunguliwa akaunti ya ChapChap ambayo mteja ufunguliwa akaunti hiyo akiwa na kitambulisho cha kupigia kura na kupewa kadi yake ya kutolea pesa kwenye mashine za NMB papo hapo na kwa gharama ya Shilingi Elfu kumi tu
 Wateja waliofika katika Moja ya gazebo lililopo nje ya Banda la Benki ya NMB katika viwanja vya sabasaba wakipata maelezo mara baada ya kufungua akaunti zao za ChapChap na kukabidhiwa kadi zao za kutolea pesa kwenye mashine za NMB papo hapo kwa gharama nafuu ya shilingi Elfu Kumi tu.
 Afisa mauzo ya Nje wa Benki ya NMB Bw Respecious Denis akitoa maelezo ya akaunti ya Chapchap kwa Mteja aliyemaliza kufungua akaunti hiyo mara baada ya kufika kwenye moja ya gazebo la Benki ya NMB lililopo katika Viwanja Vya sabasaba mapema leo
 Maafisa Mauzo ya Nje wa Benki ya NMB wakiwahudumia wateja waliofika katika gazebo la Benki ya NMB lililopo nje ya Banda la Benki ya NMB kwaajili ya Kufungua akaunti ya Chapchap ambapo mteja akimaliza kufunguliwa akaunti ukabidhiwa kadi yake ya kutolea pesa kwenye mashine za NMB papo hapo
 Maafisa Mauzo ya Nje wa Benki ya NMB wakiendelea na zoezi la kuwafungulia akaunti ya Chapchap wateja waliofika katika moja ya gazebo la Benki ya NMB kwaajili ya kufungua akaunti  ya Chapchap Kulia Ni baadhi ya Maafisa Mauzo ya Nje wa Benki ya NMB wakijiandaa kwaajili ya kumpiga Picha mteja aliyefika kwaajili ya kufungua akaunti ya Chapchap.
 Afisa Mauzo ya Nje wa Benki ya NMB Maana Katuli akimpiga picha mteja aliyefika katika Banda la NMB kwaajili ya Kufungua Akaunti ya Chapchap ambapo mteja akimaliza kufunguliwa akaunti anakabidhiwa na kadi yake ya kutolea pesa papo hapo
 Wateja wakipata maelezo ya kutosha kutoka Kwa Maafisa Mauzo ya Nje wa Benki ya NMB
 Mteja akichukuliwa alama za vidole na mmoja kati ya maafisa mauzo ya nje wa benki ya NMB waliokuwa wakimuhudumia wakati mteja huyo alipofika kwaajili ya kufungua akaunti ya Chapchap
Afisa Mauzo ya Nje wa Benki ya NMB Batuli Suna akichukua alama za vidole vya mteja alifika katika banda la benki ya NMB kwaajili ya Kufungua akaunti ya Chapchap katika Maonyesho ya 37 ya Kibiashara ya Kimataifa.