Tuesday, May 21, 2013

*TIMU 14 RCL KUUMANA RAUNDI YA PILI WIKIENDI



Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) kuwania nafasi tatu za kucheza Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu ujao inaingia raundi ya pili wikiendi hii kwa kukutanisha timu 14 zilizofanikiwa kusonga mbele.

Timu zitakazocheza raundi hiyo kwa mtindo wa nyumbani na ugenini ni Abajalo ya Dar es Salaam itakayokuwa mwenyeji Kariakoo ya Lindi katika mechi itakayochezwa Jumamosi (Mei 25 mwaka huu) Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume.

Siku hiyo hiyo Uwanja wa Azam ulioko Chamazi utatumika kwa mechi kati ya Friends Rangers ya Dar es Salaam na African Sports ya Tanga wakati Jumapili (Mei 26 mwaka huu) kutakuwa na mechi kati ya Machava FC ya Kilimanjaro na Mpwapwa Stars ya Dodoma itakayochezwa Uwanja wa Ushirika mjini Moshi.

Stand United ya Shinyanga itakuwa mgeni wa Magic Pressure ya Singida katika mechi itakayochezwa Jumapili (Mei 26 mwaka huu) Uwanja wa Namfua mjini Singida wakati Polisi Jamii ya Mara na Biharamulo FC ya Kagera zitaumana siku hiyo kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume mjini Musoma.

Mjini Kigoma kutakuwa na mechi kati ya wenyeji Saigon FC na Katavi Warriors ya Katavi. Nayo Kimondo SC ya Mbeya itakuwa mgeni wa Njombe Mji ya Njombe katika mechi itakayochezwa Jumapili kwenye Uwanja wa Sabasaba.

Mechi za marudiano zitachezwa kati ya Juni 1 na 2 mwaka huu wakati timu zitakazofuzu kucheza raundi ya tatu zitacheza mechi za kwanza kati ya Juni 8 na 9 mwaka huu wakati mechi za marudiano zitakuwa kati ya Juni 15 na 16 mwaka huu.

*JK AONGOZA KIKAO CHA CCM MJINI DODOMA LEO



  Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akizungumza na wajumbe, wakati wa Kikao Cha Kamati Kuu (CC) ya CCM, kilichofanyika leo May 21, 2013, kwenye ukumbi wa Jengo la White House, Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa CCM (Zanzibar), Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein na kulia ni Makamu Mwenyekiti wa CCM (Zanzibar), Philip Mangula na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana.
Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete na wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM, wakiwa mkutano wa Kamati hiyo, leo Mei 21, 2013,  kwenye ukumbi wa Jengo la White House, Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma. Picha na Bashir Nkoromo

Monday, May 20, 2013

*FULL MABONDIA WAKIWA NA MASHALI, MIYEYUSHO, MCHUMIATUMBO WASHINDWA KUFURUKUTA KWA TASWA FC YA LALA KWA BAO 2-1


 Kikosi cha Taswa Fc, TIMU ya Taswa Fc jana iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya timu ya Full Mabondia, inayoundwa na mabondia mahiri wa Jijini Dar es Salaam. Timu hizo zilikutana katika mchezo wa kirafiki uliochezwa kwenye Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar jana mchana, huku timu ya mabondia ikiwakilishwa na mabondia kama, Thomas Mashali, Mchumiatumbo, Francis Miyeyusho, Majia, Kanda Kabongo, na wengine wengi. Picha zote na www.sufianimafoto.com
 Wadhamini wa timu ya Taswa, Kampuni ya TSN, pia walikuwepo viwanjani hapo wakionyesha kinywaji cha Chilly Willy, kinachotengezwa na kampuni hiyo. Pichani ni baadhi ya warembo wanaotangaza bidhaa za kampuni hiyo, wakiwa katika meza yao.
 Beki wa Taswa Fc, Juma Ramadhan, (nyuma) akimdhibiti mshambuliaji wa Full Mabondia, wakati wa mchezo huo.
 Beki wa Taswa Fc, Muhidin Sufiani 'Sufianimafoto' (kulia) akimfinya mchezaji wa Full Mabondia, wakati wa mchezo huo jana.
 Beki wa Taswa Fc, Elius Kambili, akiambaa na mpira.
 Beki wa Taswa Fc, Salim (kulia) akiondosha moja ya hatari mbele ya Bondia, Mchumiatumbo.
 Kipa wa Full Mabondia, akiwa golini huku akiwa peku peku, wakati wa mtanange huo jana.
 Zahoro Milanzi wa Taswa Fc, (kushoto) akiambaa na mpira wakati wa mtanange huo.
 Wachezaji wa Taswa Fc, wakipasha kabla ya kuanza kwa mtanange huo jana.
Sufianimafoto (katikati) akipozi na Bondia Francis Miyeyusho (kushoto) na 'Chuji' (kulia) kabla ya kuanza kwa mtanange huo jana.
Benchi la Taswa Fc.

*MWASISI WA TANU, ALLY SYKES KUZIKWA LEO DAR, MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AHANI MSIBA


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimfariji mjane wa marehemu Ally Sykes, Zainab Ally, wakati alipofika kuhani msiba huo wa mwasisi wa TANU, aliyefariki jana jijini Nairobi. Marehemu Sykes anazikwa leo jioni jijini Dar es Salaam.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitia saini katika kitabu cha maombolezo ya msiba wa marehemu Ally Sykes, wakati alipofika kuhani msiba huo wa mwasisi wa TANU, aliyefariki jana jijini Nairobi. Marehemu Sykes anazikwa leo jioni jijini Dar es Salaam.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiaga na baadhi ya wazee waliohudhuria shughuli za msiba, wakati alipokuwa akiondoka baada ya kuhani msiba wa mwasisi wa TANU, Ally Sykes, aliyefariki jana jijini Nairobi. Marehemu Sykes anazikwa kuzikwa leo jioni jijini Dar es Salaam.

*REDD'S MISS KIGAMBONI WAJIFUA KUJIANDAA KUWANI TAJI JUNI 7 UKUMBI WA NAVY BEACH.


 Warembo wanaoshiriki shindano la Redd's Miss Kigamboni 2013 wakiwa kwenye mazoezi yao ya pamoja kwa ajili ya kujiandaa na kinyang'anyiro hicho kitakachotarajia kufanyika Ijumaa Juni 7 mwaka huu kwenye ukumbi wa Navy Beach Kigamboni Kigamboni.
Warembo wanaoshiriki shindano la Redd's Miss Kigamboni 2013 wakiwa kwenye mazoezi yao ya pamoja kwa ajili ya kujiandaa na kinyang'anyiro hicho kitakachotarajia kufanyika Ijumaa Juni 7 mwaka huu kwenye ukumbi wa Navy Beach Kigamboni Kigamboni.

*NGASA ALEJEA' NYUMBANI' YANGA ASAINI MKATABA WA MIAKA MIWILI,ATAMBULISHWA RASMI LEO


 KATIBU Mkuu wa Mabingwa wa Soka  Tanzania Bara, Yanga ya jijini Dar es Salaam, Lawrence Mwalusako, leo amemtambulisha rasmi Mshambuliaji mwenye mapenzi ya moyoni na timu hiyo  Mrisho Ngassa, aliyekuwa na mahasimu wao wakuu, Simba.

Mwalusako, amemtambulisha Ngassa kuwa hivi sasa ni mchezaji mpya na halali wa Yanga, baada ya kuanguka saini ya kuitumikia Klabu hiyo kwa miaka miwili, ili kuisaidia katika msimu ujao wa Ligi kuu ya Tanzania Bara na michuano ya kimataifa, inayoikabili timu hiyo baada ya kuwa mabingwa na Ligi Kuu iliyomalizika jana.



Ngassa, ameamua kurudi Yanga baada ya kuihama timu hiyo na kutimkia, Azam FC na baade kabla ya mwaka jana kuuzwa kwa mkopo, Simba, ambako amekuwa akisumbuliwa kila mara na viongozi hadi mashabiki kuwa hana mapenzi na timu hiyo na hasa kwa kitendo chake cha kubusu Jezi ya Yanga aliyorushiwa na mmoja wa mashabiki wa Yanga, katika moja ya mechi za mwaka jana wakati akiwa Azam.


Aidha Mwalusako, alisema kuwa Ngassa,  ni mchezaji wa kwanza kutangazwa na klabu hiyo na kusani mkataba wa miaka miwili ikiwa ni muda mfupi tu baada ya kumalizika kwa Ligi Kuu, ambapo ni leo ni siku muhimu iliyokuwa ikisubiriwa na Viongozi wa Yanga, Ngassa na hata mashabiki wa Yanga, waliokuwa wakiushauri uongozi kumrejesha Ngassa ''Tunduni''.  na tayari ameshaanguka saini ya kuichezea klabu yake hiyo ambayo anamapenzi nayo makubwa hapa nchini kwa miaka 2.

Ngassa, akibusu Jezi ya Yanga, baada ya kukabidhiwa na Katibu Mkuu wa Yanga,  Lawrance Mwalusako, wakati wa utambulisho rasmi uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.

*HOTUBA YA 'MR. SUGU' YAAHIRISHA KIKAO CHA BUNGE MJINI DODOMA LEO YAPIGWA 'STOP'




Hotuba ya Kambi ya Upinzani Bungeni kwa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo iliyokuwa ikisomwa na Msemaji (Waziri Kivuli wa Wizara hiyo) ambaye pia ni Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema) Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ Bungeni imesimamishwa kwa kile kilechoelezwa kukiuka taratibu za Bunge.

Akisimama kuomba Muongozo wa Spika, Mbunge wa CCM jimbo la Mbozi Mashariki, Godfrey Weston Zambi, aliliambia Bunge kuwa Hotuba hiyo katika kurasa zake 12 za awali imejaa maneno ya uchochezi kwa Serikali ya CCM.


Zambi alisema miongoni mwa maneno hayo ya Uchochezi ni yale ya kusema kuwa Serikali ya CCM kuwashambulia wanahabari kwa kuwapiga, kuwang’oa kucha, kuwamwagia tindi kali na kuwaua jambo ambalo sio kweli.

Kufuatia hatua hiyo Spika wa Bunge Anne Makinda alipokea Mwongozo huo na kuliahirisha Bunge hadi Hotuba hiyo itakapo pitiwa upya ndipo iletwe tena Bunge hapo.

Saturday, May 18, 2013

ALIEMEREMETA NA UKURASA HUU.

Ni Bi Harusi wetu Rahma akiwa na mpambe wake siku ya kitchen party yake iliyofanyika tarehe  03/05/2013 katika ukumbi wa chonya inn Ubungo River side-Dar es salaam,Picha na Nasma Mafoto.

YANGA YAMNYONYOA MNYAMA KWEUPEEEEEE, 2-0 TAIFA


 Kipa wa Simba, Juma Kaseja, akitaabika chini baada ya kushindwa kuuokoa mpira wa kichwa uliopigwa na Didier Kavumbagu, katika dakika ya 5 na kuandika bao la kuongoza katika kipindi cha kwanza. Simba nao walipata penati dakika chache baadaye baada ya Canavaro kumuangusha Ngassa katika eneo la hatari na petati ikapigwa na Mussa Mude aliyempelekea kipa katika engo ya kushoto kwake na kuokolewa na kipa huyo.  Kipindi cha pili Hamis Kiiza aliifungia Yanga bao la pili kwa kuunganisha mpira uliorushwa na Mbuyu Twite. Hadi kipute hicho kinamalizika Yanga 2, Simba 0.
Mshambuliaji wa Yanga, Simon Msuva, akichuana na beki wa Simba, Shomari Kapombe, na mpira huo ulitoka na kuwa kona iliyozaa bao. Sasa mpira ni kipindi cha pili, kaa na ukurasa huu utakaokuletea full matukio ya mechi hii ya Watani wa jadi.

Tuesday, May 14, 2013

UNESCO yaendesha warsha ya siku moja kujadili Ripoti ya hali ya Elimu na Huduma za Afya ya uzazi, maadili na mahusiano ya kingono kwa Vijana nchini

Mwenyekiti wa TACAIDS Dk. Fatma Mrisho (katikati) akizungumza wakati kufungua warsha siku moja ya mapitio na uhakikisho wa Ripoti ya hali ya Elimu na Huduma za Afya ya uzazi, maadili na mahusiano ya kingono kwa Vijana nchini ambapo warsha hiyo imeshirikisha Taasisi mbalimbali zikiwemo AMREF, UNICEF, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kutoka Tanzania Bara na Visiwani, TGNP, Wizara ya Afya na ustawi wa Jamii na nyinginezo. Kushoto ni Abdoul Coulibaly wa UNESCO na kulia ni Mwezeshaji wa Warsha hiyo kutoka Chuo kishirikishi cha Elimu cha Chuo kikuu cha Dar es Salaam (DUCE) Dr. Kitila Mkumbo.
Mwezeshaji wa Warsha hiyo kutoka Chuo kishirikishi cha Elimu cha Chuo kikuu cha Dar es Salaam (DUCE) Dr. Kitila Mkumbo akitoa mwongozo kwa washiriki wa warsha hiyo ambapo katika majumuisho yalioamuliwa kwenye warsha iliyofanyika leo ya kujadili Ripoti ya hali ya Elimu na Huduma za Afya ya uzazi, maadili na mahusiano ya kingono kwa Vijana nchini yatawasilishwa katika mkutano wa Mawaziri utakaohusisha nchi 21 za Afrika Mashariki na Kusini.
Picha juu na chini ni National Program Officer – HIV & Sexuality Education Mathias Herman kutoka UNESCO akichambua mpango wa majukumu ya nchi za Afrika Mashariki na Kusini na kutoa ufafanuzi wa matokeo ya utafiti wa Ripoti ya hali ya Elimu na Huduma za Afya ya uzazi, maadili na mahusiano ya kingono kwa Vijana nchini ambapo ameongeza kuwa nchi inatakiwa kujipanga kwa kusaidiwa na UNESCO pamoja na washirika kuongoza jitihada za kitaifa ambazo zitawawezesha washirika wakubwa ambao ni vijana kushiriki katika mikakati ya kitaifa itakayowasidia vijana nchini kujua mtazamo wao.
Pichani ni Washirki wakifuatilia uchambuzi wa Ripoti uliokuwa ukiwasilishwa na Mathais Herman kutoka UNESCO.
Mwakilishi kutoka Wizara ya Elimu na Ufundi stadi Bw. Raymond Benedict (kushoto) akikata kujua kuhusu mapitio ya Ripoti ya hali ya Elimu na Huduma za Afya ya uzazi, maadili na mahusiano ya kingono kwa Vijana nchini, huduma zinazotolewa na serikali na nini hatma na vijana wameelewa kwa kiwango gani.
Pichani juu na chini washiriki wa warsha ya siku moja iliyoandaliwa na shirika la UNESCO nchini wakichangia maoni yao.Pichani juu Katikati ni Mwenyekiti wa Asasi ya vijana ya Umoja wa Mataifa (YUNA) Lwidiko Edward akiwakilisha vijana na kulia ni Abdoul Coulibaly wa UNESCO
Picha juu na chini ni Washirki wakiendelea kufuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye warsha ya siku moja ya ya mapitio na uhakikisho wa Ripoti ya hali ya Elimu na Huduma za Afya ya uzazi, maadili na mahusiano ya kingono kwa Vijana nchini iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam na kufunguliwa na Mwenyekiti wa TACAIDS Dk. Fatma Mrisho.

Mkurugenzi wa ILO Tanzania atembelea vikundi vya jamii vinavyonufaika na mradi wa ILO wa UKIMWI kwa njia ya uwezeshaji Kiuchumi katika wilaya za Kyela na Tunduma mkoani Mbeya

Mkurugenzi wa Shirika la Kazi Kanda ya Afrika Mashariki nchini Tanzania (ILO) Bw. Alexio Musindo akikagua kinywaji aina ya ‘paw paw wine’ na mkononi akiwa ameshika matunda aina ya ‘rozela’ yanayotumika kwa kutengenezea ‘juice’ wakati alilipotembelea kikundi cha Chimbuko kinachoundwa na watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI Mjini Kyela mnamo tarehe 2, Aprili 2013 ili kujua maendeleo yao. Kikundi cha Chimbuko ni moja kati ya vikundi vya kijamii vinanvyonufaika na mradi wa UKIMWI kwa njia ya uwezeshaji Kiuchumi unaoratibiwa na ILO katika maeneo ipitayo njia kuu ya Tanzania – Zambia. (yaani Chalinze, Ilula, Mafinga, Makambako, Kyela na Tunduma).
Mwenyekiti wa kikundi Cha Chimbuko Bi Sara Mwakinyuke akimwelezea Ndugu Alexio Musindo, Mkurugenzi wa ILO Kanda ya Afrika Mashariki nchini Tanzania kuhusu matumizi ya bidhaa aina Rozela. Alifafanua pia miongoni mwa bidhaa wanazotengeneza ni pamoja na mmea wa asili aina ya mlonge ambapo alisema mlonge hutumika kama dawa inayotibu malaria. Kushoto kwake ni Afisa Mratibu Mkuu wa ILO nchini Tanzania Ndugu Anthony Rutabanzibwa aliyeongozana na Mukurugenzi wa ILO katika ziara hiyo.
Miongoni mwa vitu vilivyowashangaza maafisa wa ILO walipotembelea kikundi cha Chimbuko ni mmea wa Rozela na matunda yake kwani miongoni mwao hawajawahi kuona mmea huo bali matunda yake yakiwa tayari yameshahifadhiwa katika vifungashio. Sambamba nalo ni kitafunwa aina ya keki ya muhogo ambayo Mkurugenzi wa ILO kanda ya Afrika Mashariki alishangazwa baada ya kula keki hiyo namna ambavyo hata unga wa muhogo pia unaweza kutengenezwa keki na ikawa tamu kwelikweli!
Mkurugenzi wa Shirika la Kazi Duniani Kanda ya Afrika ya Mashariki nchini Tanzania Ndugu Alexio Musindo akiangalia bidhaa aina ya unga uitwao ‘SHIBE’ wenye mchanganyiko wa ulezi, soya lishe, mchele, karanga na mahindi unaosindikwa na kikundi cha chimbuko kama lishe bora inayoweza kutumiwa na watu wa rika zote wakiwemo wanaoishi na VVU na UKIMWI, wazee na watoto
Mwenyekiti wa vikundi cha Chimbuko Bi. Sara Mwakinyuke akimwelezea Ndugu Alexio Musindo, Mkururugenzi wa ILO Kanda ya Afrika Mashariki nchini Tanzania juu ya changamoto mbalimbali wanazokumbana nazo katika kujipatia kipato kupitia bidhaa wanazozalisha ikiwa ni pamoja na ukosefu wa vifungashio kwa ajili ya bidhaa wanazozalisha, kutoshiriki katika maonyesho ya Kitaifa ya biashara na ujasiriamali na kukosa elimu ya kutosha kuhusu uzalishaji wa bidhaa zao. Ndugu Alexio Musindo aliwaahidi kuwawezesha kupata vifungashio na Uongozi wa Halmashauri ya Kyela kupitia idara ya UKIMWI kuwaahidi kuwawezesha ili washiriki katika maonyesho ya saba saba mwaka 2013 yatakayofanyika mjini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Kikundi cha wanawake wajasiriamali cha Faith kilichopo Mjini mbeya Bi Helene Sanga akifafanua jambo baada ya kutembelewa na Ndugu Alexio Musindo, Mkururugenzi wa ILO Kanda ya Afrika Mashariki nchini Tanzania mnamo tahere 2 Aprili 2013 kuhusu bidhaa wanazotengeneza aina ya BATIKI na changamoto wanazokumbana nazo ikiwemo ufinyu wa mtaji wa kikundi ili kuweza kuzalisha aina mbalimbali za BATIKI na kushiriki katika maonyesho ya kimataifa ya kibiashara. Kikundi cha Faith ni moja kati ya vikundi vya Kijamii na Vyama vya Ushirika mjini Kyela vinavyonufaika na mradi wa UKIMWI na uwezeshaji wa Kiuchumi unaoratibiwa na ILO.
Katibu wa Kikundi cha Mshikamano wajasiriamali mjini Kyela mkoani Mbeya Bw. Nazar Mwaipasi akifafanua kuhusu maendeleo ya kikundi ikiwa ni pamoja na kuanzisha SACCOS punde baada ya kutembelewa na Ndugu Alexio Musindo, Mkururugenzi wa ILO Kanda ya Afrika Mashariki nchini Tanzania mnamo tahere 2 Aprili 2013.Bw. Nazar aliongeza kuwa kikundi cha Mshikamano kinachoundwa na wanawake na vijana wa kike na kiume wanaojihusisha na biashara binafsi na usindikaji wa vyakula kama mafuta ya mawese, samaki, mapishi na biashara ya mchele, kiliundwa baada ya mafunzo ya ujasiriamali na UKIMWI yaliyotolewa kwa wanawake na vijana kupitia mradi wa UKIMWI na uwezeshaji wa Kiuchumi wa ILO.

NMB YATUNUKIWA KWA KUFADHILI MKUTANO MKUU WA 29 WAJUMUIYA ZA TAWALA ZA MITAA TANZANIA


 Waziri Mkuu Mizengo Pinda, akimkabidhi Cheti, Mkuu wa Idara ya Mahusiano Biashara ya Serikali NMB, Domina Feruzi,  kama ishara ya shukrani kwa  benki ya NMB kwa kuwa mdhamini mkuu wa Mkutano Mkuu wa 29 wa Jumuia za  Tawala za Mitaa Tanzania uliofanyika mwishoni mwa wiki jijini Arusha.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akisalimiana na Maofisa wa benki ya NMB alipotembelea banda la benki hiyo wakati wa mkutano wa 29 wa Jumuia za  Tawala za Mitaa Tanzania uliofanyika mwishoni jijini Arusha. 
 Waziri Mkuu Mizengo Pinda akipokea kadi ili kujionea kadi hiyo ya Chapchap baada ya kupata maelezo kutoka kwa Ofisa wa NMB Balthazar Clemence wakati wa mkutano wa 29 wa Jumuia za  Tawala za Mitaa Tanzania uliofanyika mwishoni mwa wiki jijini Arusha.

WANYWAJI WAPINGA VIROBA KUPIGWA MARUFUKU, ''Vikipigwa marufuku viroba tutarudi kunywa gongo''-WANYWAJI


Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Viwanda na Biashara, wakiangalia uzalishaji walipotembelea kiwanda cha Konyagi cha Tanzania Distilleries Limited (TDL), Dar es Salaam hivi karibuni.
**********************
 Na Mwandishi Wetu.
BAADHI ya wananchi jijini Dar es Salaam, wamelalamikia hoja iliyozuka bungeni wiki hii kwamba kinywaji cha Konyagi aina ya Kiroba kipigwe marufuku nchini.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi hao, walisema endapo serikali itachukua uamuzi wa kupiga marufuku kinywaji hicho, watarudia kunywa pombe aina ya gongo ambayo ni hatari kwa afya zao.

Mkazi wa Mbagala, Faustine Mwiruka aliyekutwa kwenye baa ya Kisuma, aliiasa Serikali kutothubutu kukubali kinywaji hicho kupigwa marufuku, kwani ikifanya hivyo wengi wa wananchi wenye kipato cha chini wataanza tena kunywa gongo na pombe za kienyeji.

Itabidi tufanye kama Zambia  ambao wamezuia viroba, lakini nchi nzima imejaa viroba vya Malawi, Zaire na Burundi, lazima tuiadhibu serikali ikose kodi kote kote, bia hatunywi, viroba vya nje tutakunywa, pamoja na gongo.

Alisema haingii akilini kukihusisha kinywaji hicho na ajali za magari, akidai kuwa hata kabla ya viroba kuingia sokoni ajali zilikuwepo nyingi.

"Sisi tuna imani na viroba kwa vile vina ubora wa uhakika tofauti na pombe ya gongo ambayo inapikwa bila kupimwa ubora hivyo ni hatari kwa usalama wa afya zetu." alisema Mwiruka.

Naye Ali Hassan mkazi wa Kinondoni kwa Manyanya, alisema, wanaotaka viroba vipigwe marufuku hawawatendei haki wananchi wa kawaida ambao kwa asilimia kubwa hawana uwezo wa kununua bia ambazo bei yake ni kubwa.

Mwandishi wetu aliyetembelea maeneo ya Ilala Kota Mchikichini alifanikiwakuhojiana na wakazi wa eneo hilo ambao wengi wao walisema kuwa jambo hilo lililozushwa wiki iliyopita wanaamini ni njama za wafanya biashara toka nchi jirani ambao hawaitakii mema Tanzania  kwa kuwa pombe hiyo kuwepo kwake pia kunakuza pato la Taifa.

Juma Pingu alisema kuwa haoni sababu ya kupiga marufuku viroba kwakuwa ni pombe ya wanyonge na kuwataka wabunge kuthamini bidhaa za nyumbani kwanza.

Akizungumza na waandishi wa habari mwanzoni mwa wiki hii, Mkurungenzi Mkuu wa Konyagi, David Mgwassa alisema kuwa kwa kipindi kirefu kumekuwa na mchezo mchafu wa kuharibiana jina sokoni kwa kutumia baadhi ya vyombo vya habari vya hapa nchini, kampeni inayoendeshwa na makampuni yenye uhusiano na makampuni makubwa ya pombe duniani yasiyo penda, nchi za afrika zizalishe pombe zake, bali ziendeleee kununua kutoka Ireland, wales. Kenya  and uingereza.

Wadau hao wa Pombe nchini walifikia uamuzi wa kutoa maoni hayo baada ya kuona kuwa kinywaji chao Kiroba kinapigwa vita lukuki kwenye magazeti. Huwezi ukahusisha viroba na piki piki, kwani nchi hii ina piki piki laki tatu, na wananchi million 43, uhusiano wake uko wapi, kwanza hata leseni hamuwapi?