Tuesday, March 25, 2014

*KASEBA NA MASHALI NANI ZAIDI WA MANZESE V/S MWANANYAMALA

MARASTA WAKUTANISHWA, Japhet Kaseba (kushoto) akipozi na Thomas Mashali, wakati wa utambulisho wa pambano lao la jumamosi.
****************************************************
Hivi karibuni watakutanishwa miamba miwili ulingoni wote wakiwa na nywele zilizotengenezwa kwa mtindo wa rasta, Miamba hiyo  ambayo mara nyingi huwa gumzo la watu mitaani hususani wapenda mchezo wa ngumi kwa tabia zao na vibweka vyao , hao si wengine bali ni Japhet kaseba na bondia mtukutu Thomas Mashali, ambao  jumamosi ya terehe 29/3/2014 watapanda ulingoni katika ukumbi  PTA viwanja wa maonesho sabasaba, kuonyeshana kazi.
 Thomas  mashali “simba asiyefugika – kama anavojiita” alizaliwa sept 1989 na kukulia mitaa ya manzese jijini Dare s salaam, akiwa mtoto mtundu, mkorofi, mgomvimgovi  na mpenda michezo kama ilivyo kwa mdogo wake Charles Mashali, ambaye pia  alikuwa  bondia mzuri aliyetokea kuwashinda na  kuwasumbua mabondia wengi kama kina Francis Miyeyusho, alishawahi kuchukua ubingwa wa taifa kabla ya kuachana na mchezo wa ngumi.
Mashali amewahi kuwa kivutio cha wengi  ulingoni na kero kwa wengine uraiani kwa tabia yake ya kuwapigapiga  watu na kuwaonea wasio na hatia na kuendekeza ubabe usio na maana akiwa kama tembo wa mitaa ya manzese kwa tabia yake iliyomfanya kwenda jela  mara kwa mara na kumpotezea dira imara katika masumbwi  na kukaa muda mrefu bila kupigana.
Mwaka 2009 alipotokea jamaa mmoja anayeitwa juma shumbili ambae ni promota wa mapambano madogomadogo ya mchangani lakini kwa wakati huu alikuwa anaandaa zaidi katika ukumbi wa texas hall manzese na kumuandalia pambano Thomas mashali akiwa kama mbabe wa manzese na amadu mwalimu akiwa kama  mbabe wa tandika.
Matokeo Mashali aliibuka mshindi  wa pambano hilo kwa kumpiga amadu mwalimu kwa no kaunti ya raundi ya tatu na hili ndilo pambano lake la kwanza rasmi la kulipwa  lililomuingiza katika rekodi ya mabondia  wa kulipwa nchini.
Sasa, Jumamosi Mashali niuso kwa uso na Japhet Kaseba, nani kuibuka kidedea?????

*BREAKING NEEEEEWZZZ!!!!!! MKUU WA MKOA MARA JOHN TUPA AFARIKI GHAFLA


Habari zilizoufikia mtandao huu hivi punde zinasema kuwa, John Tupa, Mkuu wa Mkoa wa Mara, (pichani) amefariki ghafla muda mchache uliopita. Kwa mujibu wa mtoa habari ni kuwa marehemu Tupa, alikuwa akitoka katika moja ya kikao cha utendaji mkoani kwake ambapo baada ya kupewa 'Breafing', sasa alikuwa akielekea eneo husika kwa ajili ya kutembelea na kukagua kile alichoeleza katika taarifa hiyo, na wakati akipanda gari ndipo alipoanguka na kupoteza maisha. Mungu ametoa na Mungu ametwa, Mungu ilaze roho ya Marehemu Tupa mahala pema pepon, Amina.

Habari zitawajia kwa kadri zitakavyotufikia

Saturday, March 22, 2014

HOTEL YAWAKA MOTO-DAR


Hotel ya Picolo-Iliyopo kawe imewaka moto leo majira ya mchana,chanzo cha moto huo inasemekana ni shoti ya umeme!

KIM KARDASHIAN,KANYE WEST COVER VOGUE;‘This is such a dream come true’














SHARE THIS URL

 Kim Kardashian and Kanye West are on the cover of the April 2014 issue of Vogue.
ANNIE LEIBOVITZ/VOGUE
Kim Kardashian and Kanye West appear on the April cover of Vogue, which hits newsstands March 31.
Kim Kardashian's Vogue dream has finally come true.
After months and months of speculation, the reality starlet covers the April issue of the high-end fashion magazine in the arms of her husband-to-be, Kanye West.
Kardashian, 33, stuns in a white Lavin gown resembling a wedding dress just ahead of the couple’s upcoming nuptials slated for this May in Paris, France. West dons a Saint Laurent blazer.

 Behind the scenes look at Kim Kardashian and Kanye West's cover shoot for Vogue.
VOGUE.COM
The adorable North West joined her parents for their Vogue cover shoot.
The gorgeous shots were taken by famous photographer Annie Leibovitz.
"This is such a dream come true!!! Thank you @VogueMagazine for this cover! OMGGGGGG!!! I can't even," Kardashian tweeted Friday along with a pic of the magazine.

RAIS JK KUKUTANA NA WATANZANIA WAISHIO UINGEREZA JUMAPILI YA TAREHE 30 MACHI 2014

Ubalozi wa Tanzania London - Uingereza, unafuraha ya kuwatangazia Watanzania wote waishio Uingereza kuwaMhe. Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, atakutana na Watanzania siku ya Jumapili tarehe 30 Machi 2014.

Mkutano huo utafanyika katika ukumbi wa Sattavis Patidar Centre, Forty Avenue, Wembley Park, London, Middx, HA9 9BE, kuanzia saa 10 jioni (16:00).

Katika Mkutano huo, Mhe.Rais Kikwete atazungumzia maendeleo ya nchi yetu na pia kutumia fursa hiyo kusikia masuala yanayogusa maslahi ya wanadiaspora. 

Mhe. Rais atakuwa nchini Uingereza kuanzia tarehe 30 Machi hadi 2 April 2014 kwenye ziara ya kikazi kwa mwaliko rasmi wa Waziri Mkuu wa Uingereza, Mhe. David Cameron.

Ubalozi unapenda kuchukua fursa hii kuwaomba Watanzania wa maeneo ya Uingereza na nchi jirani kujitokeza kwa wingi kumkaribisha Rais kwenye Mkutano huu adimu.


Kwa Taarifa zaidi:
Simu: 0207 569 1470
Email: balozi@tanzania-online.gov.uk

Ahsanteni sana- Ubalozi wa Tanzania – London

BOFYA HAPA KUCHEKI "MSAMBINUNGWA" YA TUNDAMAN & ALIKIBA

Wednesday, February 26, 2014

*HABARI KUTOKA TFF LEO

*SYMBION KUSAIDIA PROGRAMU ZA VIJANA TFF
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na Symbion Power Tanzania Limited zimesaini makubaliano ambapo kampuni hiyo itasaidia kwenye maeneo matatu ya mpira wa miguu wa vijana.

Makubaliano hayo yametiwa saini leo (Februari 26 mwaka huu) kwenye ofisi za TFF jijini Dar es Salaam. Rais wa TFF, Jamal Malinzi amesaini kwa niaba ya shirikisho wakati upande wa Symbion aliyesaini ni Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo Peter Gathercoles.

Maeneo ambayo Symbion itasaidia ni ujenzi wa vituo viwili vya kuendeleza vipaji vitakavyojengwa Kidongo Chekundu na Kinondoni mkoani Dar es Salaam, mashindano ya Taifa ya wachezaji wenye umri wa chini ya miaka 12 (U12) yatakayofanyika mwaka huu na kuisaidia timu ya U17 ya Tanzania (Serengeti Boys).

Serengeti Boys itacheza na Afrika Kusini, Julai mwaka huu katika mechi za mchujo kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika kwa wachezaji wa umri huo zitakazofanyika mwakani nchini Niger.

Hivyo Symbion imetoa dola 60,000 (zaidi ya sh. milioni 96) kwa ajili ya mashindano ya U12, na dola 50,000 (zaidi ya sh. milioni 80) kwa ajili ya maandalizi ya Serengeti Boys kwa mechi dhidi ya Afrika Kusini.

Rais Malinzi ameishukuru Symbion kwa kukubali kushirikiana na TFF katika mpira wa miguu wa vijana, lakini vilevile amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete kwani ndiye chachu ya kampuni hiyo kuamua kujishirikisha na mpira wa miguu wa vijana.

*ZAMBIA WATUA KUIKABILI TWIGA STARS
Timu ya Taifa ya Zambia (Shepolopolo) inatua nchini kesho mchana (Februari 27 mwaka huu) kwa ajili ya mechi ya marudiano ya michuano ya Afrika kwa Wanawake (AWC) dhidi ya Tanzania (Twiga Stars) itakayochezwa keshokutwa (Februari 28 mwaka huu).

Shepolopolo yenye msafara wa watu 29 itawasili kwa ndege ya Fastjet ikitokea Lusaka na itafikia kwenye hoteli ya Accomondia kwa ajili ya mechi hiyo itakayochezwa Uwanja wa Azam Complex ulioko Chamazi kuanzia saa 10 kamili jioni.

Waamuzi wa mechi hiyo kutoka Burundi wakiongozwa na Ines Niyosaba wamewasili nchini leo asubuhi wakati Kamishna Fran Hilton-Smith kutoka Afrika Kusini atawasili kesho (Februari 27 mwaka huu) saa 8 kamili mchana kwa ndege ya South African Airways.

*RAIS MALINZI KUZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi atakuwa na mkutano na waandishi wa habari juu ya benchi la ufundi la timu ya Taifa ya wakubwa (Taifa Stars).


Mkutano huo utafanyika kesho (Februari 27 mwaka huu) saa 4 asubuhi kwenye ofisi za TFF zilizopo ghorofa ya 3 katika Jengo la PPF Tower, mtaa wa Garden na Ohio.

*CHAMA cha Mapinduzi (CCM), chajiingiza matatani baada ya kuwapangisha wafanyabiashara wawili katika flemu moja

indexCHAMA cha Mapinduzi (ccm), kimejiingiza matatani baada ya kuwapangisha wafanyabiashara wawili katika flemu moja ya kufanyia biashara.  Akizungumza jana jijini Dar es Salaam mfanyabishara Charles Msigwa alisema aliingia mkataba na Mecy Mziray ambaye kwa sasa ni marehemu na aliendelea kumlipa kodi ndugu wa marehemu Vesta Haule. 

Alisema wakati akiendelea kufanya biashara katika banda hilo alishangazwa na viongozi wa CCM tawi la Vigaeni Kata ya Ndugumbi kumfuata wakitaka aingie mkataba upya na chama hicho. 

“Nimekuwa nikiendesha shughuli zangu za biashara kwa muda wa miaka minne ndipo nilipofuatwa na viongozi wa CCM na kunishauri nichukue mkataba nao ili chama kipate mapato,”alisema Msigwa. 

Aliongeza kuwa viongozi hao walimuita kwenye ofisi ya tawi na kumuhakikishia hakutakuwa na tatizo lolote juu ya mkataba huo. “Viongozi hao waliniambia kuwa mabanda hayo hayarithishwi hata hivyo aliyeachiwa amekuwa msumbufu wa kodi mwenye banda alishafariki kwa hiyo banda huwa linarudi na kuwa mali ya chama,”alisema. 

Msigwa alisema kuwa aliujaza mkataba huo na kuurudisha ofisini kwao alipotaka kuulipia akawa anazungushwa zungushwa. 

“Nilipeleka malalamiko yangu Kwa uongozi wa Wilaya ambapo uliwaandikia barua ya kwamaba wanitafutie banda jingine iwapo nikiwa tayari kutimiza masharti ya kuwa mpangaji wa chama hicho na nilikubali lakini uongozi huo haukufanya kama ulivyo agizwa,”alisema Msigwa. 

Awali Chama cha mapinduzi (CCM) kiliingia mkataba wa kujenga banda hilo na Marehemu Mecy Mziray gharama zake na asingeweza kutoka mpaka gharama zake za ujezi zitakapo malizika.

Monday, January 6, 2014

BOFYA HAPA UCHEKI MY NUMBER ONE REMIX YA DIAMOND FT DAVIDO

Number One Diamond and Davido

*MIONDOKO YA HARUSI YA MOHAMED NA ELIZABETH


KWA MAHITAJI YAKO KATIKA SHUGHULI ZA SHEREHE KAMA VIDEO, PICHA, MUZIKI NA MC'S PIA KAVA DISGN, VIDEO EDITING N.K WAWEZA KUWASILIANA NASI KWA:-

SIMU NO:- 0752 882038/0714656660/0784782038 au 0655 306109/0787 200005/0754306109
BARUA PEPE:- muhidinuk@yahoo.co.uk,sufianimafotoblog@gmail.com

WEBSITE:- www.sufianimafoto.com, www.nasmamafoto.blogspot.com

Sunday, January 5, 2014

*RAIS KIWETE ALIPOPOKEA MATEMBEZI YA UVCCM ZANZIBAR JANA

 Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete akikagua gwaride la Chipukizi kabla ya kupokea maandamano ya watembeaji  kusherehekea miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar katika viwanja vya Maisara mjini Zanzibar, jana.
 Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete akipokea maandamano ya watembeaji  kusherehekea miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar katika viwanja vya Maisara mjini Zanzibar.
 Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete akikagua Brass Band ya  Chipukizi kabla ya kupokea maandamano ya watembeaji  kusherehekea miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar katika viwanja vya Maisara mjini Zanzibar.
 Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete akipokea maandamano ya watembeaji  kusherehekea miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar katika viwanja vya Maisara mjini Zanzibar.
 Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na wana UVCCM baada ya  kupokea maandamano ya watembeaji  kusherehekea miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar katika viwanja vya Maisara mjini Zanzibar.
 Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete, Makamu wa Mwenyekiwa CCM (Visiwani) na Rais wa Zanzibar  Dkt Ali Mohamed Shein na Viongozi wengine waki imba wimbo wa mashujaa wakati wa  ya kupokea maandamano ya watembeaji  kusherehekea miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar katika viwanja vya Maisara mjini Zanzibar.
Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete akihutubia baada ya  kupokea maandamano ya watembeaji  kusherehekea miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar katika viwanja vya Maisara mjini Zanzibar. PICHA NA IKULU

Saturday, December 21, 2013

*SIMBA BILA OKWI & KASEJA INAWEZEKANA! YAICHAPA YANGA 3-1


 Kocha Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic, akiruka hewani kushangilia bao la kwanza la Simba lililofungwa na Hamis Tambwe katika dakika ya 14, ya kipindi cha kwanza.
 Mshambuliaji wa Simba Hamis Tambwe, akifunga bao la pili kwa mkwaju wa penati katika dakika ya 44, baada ya beki wa Yanga, David Luhende kumkwatua Ramadhan Singano katika eneo la hatari.
Mshambuliaji wa Yanga, Didier Kavumbagu, akijaribu kumfinya beki wa Simba, Joseph Owino wakati wa mtanange huo. Mpira sasa ni kipindi cha pili

Saturday, September 7, 2013

BOFYA HAPA NYIMBO MPYA YA DIAMOND-MY NUMBER 1

KUNANI JUSTIN BEIBER NA PARIS JACKSON

Baadhi ya watu wajiuliza ukaribu wao

*STARS YAWASILI BANJUL, KUIVAA GAMBIA LEO



Na Boniface Wambura, Banjul +2207362384
Kikosi cha Taifa Stars kimewasili salama hapa Banjul, Gambia tayari kwa mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya wenyeji itakayochezwa leo Septemba 7.

Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager imewasili hapa jana (Septemba 5 mwaka huu) saa 11 jioni ikitokea Dakar, Senegal ambapo ilichelewa kuunganisha ndege, hivyo kuamua kutumia usafiri wa barabara kwa vile ni karibu na baadaye kupanda kivuko kuingia Banjul badala ya kulala na kuchukua ndege nyingine siku inayofuata.

Wachezaji wako katika hali nzuri na leo jioni wanatarajia kufanya mazoezi ya mwisho kwenye Uwanja wa Independence ulioko Bakau ambao utatumika kwa mechi ya kesho. Timu imefikia hoteli ya Seaview iliyoko kandokando ya Bahari ya Atlantic.

Mechi hiyo itaanza saa 10.30 jioni kwa saa za hapa ambapo nyumbani Tanzania itakuwa saa 1.30 usiku, na itachezeshwa na waamuzi kutoka Rwanda Munyemana Hudu. Waamuzi wasaidizi ni Theogene Ndagijimana, Honore Simba na Issa Kagabo. Kamishna ni Andy Quamie kutoka Liberia.
Washabiki na vyombo vya habari vya hapa wanaizungumzia mechi hiyo ambayo ina umuhimu mkubwa kwa pande zote, huku Gambia ikiwa imeita wachezaji tisa wanaocheza barani Ulaya na Marekani. Gambia ambayo imepata uongozi mpya wa Chama cha Mpira wa Miguu Gambia (GFA) imepania kuhakikisha haimalizi mechi za mchujo ikiwa na pointi moja tu.

Kwa upande wa Tanzania, Kocha Kim Poulsen amesema nia ni kuona Stars yenye pointi sita inamaliza katika nafasi ya pili nyuma ya Ivory Coast ambayo tayari imechukua tiketi pekee ya kucheza raundi ya mwisho kutoka kundi hili la C.

“Mechi hii ni muhimu kwetu kwa vile tunataka matokeo mazuri ugenini. Lakini kikubwa ni kuwa matokeo mazuri si tu yatatuweka katika nafasi ya kuwa wa pili, lakini vilevile yatatusaidia kuongeza pointi kwenye viwango vya ubora vya FIFA, na kikubwa zaidi hii ni sehemu ya maandalizi ya sisi kucheza Fainali za Afrika za 2015,” amesema Kim.

Stars inatarajiwa kupangwa hivi; Juma Kaseja, Vincent Barnabas, Erasto Nyoni, Nadir Haroub, Henry Joseph, Frank Domayo, Haruni Chanongo, Amri Kiemba, Mrisho Ngasa, Simon Msuva na Khamis Mcha

*REDD'S MISS TANZANIA 2013 WATEMBELEA RADIO 5 YA JIJINI ARUSHA



Mtangazaji wa kipindi cha burudani cha Funika Base kutoka Radio 5 ya Mjini Arusha , Julius Kamafa (kushoto) akifanya mahojiano na Washiriki wa Shindano la Redd’s Miss Tanzania 2013 katika studio za redio hiyo jana.
 Baadhi ya warembo wakijieleza Live Redio 5 hii leo walipotebelea kituo hicho. KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPO CHINI

FIESTA KUWASHA MOTO MBEYA.



Msanii wa muziki wa kizazi kipya,ambaye kwa sasa anafanya vyema kwenye anga za muziki huo,Neylee akiimba kwa hisi jukwaani huu wakati tamasha la Serengeti Fiesta likiendelea kwa shangwe ndani ya uwanja wa Sokonine.
Wakazi wa jiji la Mbeya wakiwa wamejitokeza kwa wingi usiku huu kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2013 ndani ya uwanja wa Sokoine,ndio kwanza shoo inaanza ambapo msanii aliyewahi kuiwakilisa shindano la BSS,Walter Chilambo ndiye aliyefungua pazia la onesho hilo usiku huu. 

 Tamasha la Serengeti Fiesta 2013 likiendelea usiku huu kwenye uwanja wa Sokoine,Mkoani Mbeya
 Mama wa miduara ya Kibongofleva,Shilole akiwa na madensa wake wakitumbuiza jukwaani usiku huu ndani ya tamasha la Serengeti fiesta 2013,ndani ya uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya. KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPO CHINI