Sunday, November 23, 2014

BALOZI SEIF IDDI ZIARAN NCHINI CHINA


 Ujumbe wa Zanzibar uliokuwa nchini China kwa ziara ya Kiserikali ukipata mlo kwenye Tafrija  maalum waliyoandaliwa na Ubalozi wa Tanzania Nchini China.
Wa kwanza kutoka kushoto ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mh. Said Hassan Said, Meya wa Manispaa ya Zanzibar Mstahiki Khatib Abdulrahman Khatib, Waziri wa Ardhi, Makazi, Maji na Nishati Mh. Ramadhan Abdulla Shaaban,Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo Mh. Said Ali Mbarouk na Mwakilishi wa Jimbo la Chaani Mh. Ussi Jecha Simai.
 Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Suleiman Iddi akiwa pamoja na Mke wa Balozi wa Tanzania Nchini China Mama Mary  Antony  Tairo pamoja na Afisa wa Ubalozi huo Nd. Kitokezi Juma Kitokezi wakiwa kwenye Tafrija iliyoandaliwa na Ubalozi wa Tanzania Nchini China kwa ujumbe wa Zanzibar.
  Mkuu wa Ufundi wa Kampuni ya Kimataifa ya Ujenzi ya China { BCEG } Mhandisi  Tiger Nzu akimpatia maelezo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi na ujumbe wake ulipofanya ziara ya kutembelea uwanja wa Kimataifa wa Beijing Nchini China ambao umejengwa na Kampuni hiyo ya BCEG.
Nyuma ya Mhandisi Tiger Nzu  ni Waziri wa Habari Utamaduni, Utalii na Michezo Mh. Said Ali Mbarouk, kati kati ya Balozi Seif na Mh. Said ni Mkurugenzi wa Idara ya Mambo ya Nje Zanzibar Balozi Silima Kombo, kushoto ya Balozi Seif ni Waziri wa Ardhi, Makazi, Maji na Nishati Mh. Ramadhan Abdulla Shaaban na nyhuma yake ni Mwakilishi wa Jimbo la Chaani Mh. Ussi Jecha Simai.
Balozi Seif akizungumza mara baada ya Tafrija iliyoandaliwa na Kampuni ya Ujenzi ya BCEG kwa ajili ya Ujumbe wake baada ya kumaliza kutembelea uwanja wa ndege wa Beijing Nchini China.
Mbele ya Balozi Seif aliyevaa miwani na kukaa ni Naibu  Meneja wa Kampuni ya BCEG Bwana Dinng Chuanbo.

Picha na Hassan Issa wa – OMPR – ZNZ.
                 Press Release:-
Mashirika Taasisi za Umma na zile binafsi pamoja na wazazi wanaowadhamini kimasomo wafanyakazi na watoto wao Nchini Jamhuri ya Watu wa China wanapaswa kuwasiliana na  Uongozi wa Ubalozi wa Tanzania Nchini humo ili kuepuka utapeli unaofanywa na baadhi ya mawakala wa sekta hiyo.
Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Nchini China Balozi Abdulrahman Amir Shimbo alitoa kauli hiyo wakati wa dhifa maalum aliyouandalia Ujumbe wa Zanzibar ulioongozwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi  ulipofanya  ziara yake Nchini humo.
Dhifa hiyo iliyoshirikisha pia wafanyakazi wa Ubalozi huo ilifanyika katika Ofisi ya Ubalozi Wa Tanzania uliopo katika Bara bara ya Liang Ma He Naulu Mtaa wa Sanlitum Mjini Beijing Nchini China.
Balozi Shimbo alisema yapo matatizo mengi yanayoendelea kuwakumba Wanafunzi wengi wanaotoka Tanzania kwa kutumia Mawakala wababaishaji licha ya kwamba baadhi yao wamepata ufadhili usio na usumbufu.
Alisema kitendo cha baadhi ya wafadhi  pamoja na wazazi wa wanafunzi hao kutumia mawakala husababisha kuibuka kwa matatizo na gharama kubwa zinazoweza kuepukwa sambamba na kuuongezea mzigo Ubalozi.
Balozi Abdulrahman alieleza kwamba hivi sasa wanafunzi wengi wanapata fusa za masomo Nchini China ambapo wengi kati yao hupata ufadhili wa Serikali, Taasisi na Mashirika ya Umma pamoja na Wazazi binafsi.
Balozi huyo wa Tanzania Nchini China aliuelezea ujumbe huo wa Zanzibar kwamba  mwaka ujao Serikali ya Jamuhuri ya Watu wa China imeongeza nafasi 100 za masomo ya juu kwa Wanafunzi wa Tanzania kupata taaluma ya vyuo vikuu mbali mbali Nchini humo.
Alifahamisha kwamba Ofisi yake itawasiliana na Serikali zote mbili ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na ile ya Mapinduzi ya Zanzibar  katika uratibu wa kuzitumia nafasi hizo ili ziwafaidishe Vijana wa pande zote mbili za Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.
Akigusia ziara mbali mbali za Viongozi wa ngazi za Juu wa Tanzania wanaotembelea China Balozi Shimbo alisema Wafanyakazi wa Ofisi ya Ubalozi huo wamepata faraja kubwa kufuatia ujio wa Viongozi hao.
Balozi Shimbo alisisitiza kwamba Uongozi wa Ubalozi huo unaendelea kufuatilia utekelezaji wa makubaliano au ahadi zilizotolewa kufuatia ziara za Viongozi hao wakuu wa Tanzania  China.
Alisema ziara hizo kwa pande zote mbili kati ya china na Tanzania kwa kiasi kikubwa zimeleta na  kuimarisha zaidi uhusiano uliopo kati ya pande hizo mbili rafiki.
Akitoa shukrani kwa niaba ya ujumbe aliouongoza Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi aliwakumbusha wafanyakazi wa Ubalozi huo wa Tanzania Nchini China kuzidisha mashirikiano yao kwa lengo la kupata ufanisi zaidi.
Balozi Seif alisema mashirikiano hayo yataendeleza sifa ya watendaji hao kufanya kazi katika misingi ya umoja na upendo kama utamaduni wao ulivyowalea na kuwanyooshea njia.
Akigusia ziara yao nchini China Balozi Seif alisema ujumbe wake umeona na kushuhudia maendeleo makubwa yaliyofikiwa na China katika kukuza uchumi na kuimarisha maendeleo ya ustawi wa Jamii.
Alisema licha ya kujifunza huko lakini pia ziara ya ujumbe huo wa Zanzibar imesaidia kuimarisha uhusiano wa kihistoria unaoendelea kukua siku hadi siku kati ya China na Tanzania na Zanzibar kwa jumla.
Alifafanua kwamba Zanzibar na China hasa kisiwa cha Jimbo la Hainan zimekuwa na mafungamano makubwa ya ushirikiano wa muda mrefu uliokuja kutokana na kufanana kwa mazingira ya visiwa hivyo viwili vilivyoko katika ukanda wa joto.
Balozi Seif alimuhakikishia Balozi wa Tanzania Nchini China Balozi Abdulrahman Shimbo kwamba mambo yaliyokubalika ndani ya ziara hiyo yatafuatilia ili kuona ufanisi unapatikana.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliwapongeza Wafanyakazi wa Ubalozi huo kwa dhifa maalum waliyouandalia ujumbe wake jambo ambalo ni moja kati ya  utamaduni uliojengeka miongoni mwa Watanzania.
Mapema Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi na Ujumbe wake walipata fursa ya kutembelea maegesho ya ndege katika uwanja wa Kimataifa wa Beijing sehemu ya Tatu { Terminal Three } iliyojengwa na Kampuni hiyo ya Beijing Construction Engeneering Group.
Mkuu wa ujenzi  wa Kampuni hiyo Mhandisi Tiger Nzu aliueleza ujumbe huo wa Zanzibar kwamba uwanja huo wenye urefu wa kilomita tatu una sehemu 96 zenye uwezo wa kuhudumia abiria mbali mbali wa safari za Kitaifa na Kimataifa.
Mhandisi Tiger alifahamisha kwamba huduma zote zinazopaswa kupatiwa abiria wakiwemo walemavu na watu wenye mahitaji maalum kama watoto a Wagonjwa zimepangiwa utaratibu maalum katika viwango vinavyokubalika Kimataifa.
Wakati  wa Tafrija ya chakula cha mchana iliyoandaliwa na Kampuni hiyo ya BCEG Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema kwamba uzoefu na utaalamu mkubwa uliyonayo Kampuni ya Kimataifa ya ujenzi ya Jamuhuri ya Watu wa China { Beijing Construction Engeering Grouop -BCEG } unatoa matumaini makubwa kwa kumalizika kwa mafanikio uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Zanzibar.
Alisema kazi kubwa inayoendelea kufanywa na Kampuni hiyo inayojenga maegesho ya uwanja wa ndege wa Zanzibar inatoa matumaini ya kuufanya uwanja huo kufikia hadhi ya Kimataifa.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliupongeza Uongozi na Wafanyakazi Kampuni hiyo ya { BCEG } kwa umakini wake ambao ndio saabu unayoupa fursa nyingi za tenda za ujenzi kampuni hiyo katika Mataifa mbali mbali Duniani hasa nchi za Bara la Afrika.
Naye Naibu Meneja wa Kampuni ya Ujenzi ya BCEG Bwana Ding Chuanbo alisema kukamilika kwa ujenzi wa maegesho ya ndege kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Zanzibar kutaiwezesha Zanzibar kupiga hatua kubwa za kimaendeleo.
Bwana Ding alisema mabadiliko ya Kiuchumi ya Zanzibar yatazidi kuimarika kufuatia kuongezeka kwa mapato kupitia sekta ya Utalii inayoonekana kuchukuwa nafasi ya juu katika uchumi wa Zanzibar.
Naibu Meneja huyo wa Kampuni ya BCEG aliueleza ujumbe huo wa Zanzibar kwamba Kampuni hiyo iliyoasisiwa mwaka 1953 tayari imefanikiwa kiuzalishaji  hali inayoifanya kuwa na Idara 24 za fani tofauti za utaalamu.
Balozi Seif na Ujumbe wake amemaliza ziara yake Nchini Jamuhuri ya Watu wa China akipitia Mjini Dubai kwa mapumziko mafupia ambapo anatarajiwa kurejea nyumbani mwisho mwa wiki hii.
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
23/11/2014.

Friday, November 21, 2014

MAADHIMISHO YA SIKU YA UKIMWI DUNIANI KUFANYIKA KITAIFA MKOANI NJOMBE

Mwenyekiti Mtendaji wa Tume ya Taifa ya kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS) , Dkt. Fatma Mrisho akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari kuhusu Kauli Mbiu ya Maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani isemayo, Tanzania Bila Maambukizi Mapya ya VVU, Vifo vitokanavyo na Ukimwi na Ubaguzi na Unyanyapaa inawezekana inayolenga kupunguza maambukizi Mapya ya Ukimwi, kupunguza vifo vitokanavyo na Ukimwi na kukomesha vitendo vya unyanyapaa kwa asilimia Sifuri. 
Mkurugenzi wa ufuatiliaji wa Tathmini wa Ofisi ya Taifa ya kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS) Dkt. Jerome Kamwela akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari kuhusu utoaji wa huduma na upatikanaji wa dawa za kufubaza makali ya Virusi vya Ukimwi kwa watu wanaoishi na VVU katika maeneo mbalimbali nchini.
Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa TACAIDS akiwaonesha waandishi wa habari (hawapo pichani) mbinu na elimu inayotolewa na TACAIDS katika maeneo mbalimbali ikiwemo matumizi ya mipira ya kike kwa wanawake ili kuzuia maambukizi mapya ya VVU. Picha na Aron Msigwa - MAELEZO
Maadhimisho ya siku ya UKIMWI Duniani kwa mwaka 2014 kitaifa yanatarajiwa kufanyika mkoani Njombe kuanzia tarehe 24 mwezi huu hadi tarehe  moja  Desemba.
Hayo yamesemwa leo na Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Taifa ya kudhibiti UKIMWI (TACAIDS) Dkt. Fatma Mrisho wakati akiongea na waandishi wa habari katika ukumbi wa mikutano uliopo makao makuu ya tume hiyo jijini Dar es Salaam.
Dkt. Mrisho amesema kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni “Tanzania bila maambukizo mapya ya Virusi Vya Ukimwi (VVU), Vifo vitokanavyo na UKIMWI, Ubaguzi na unyanyapaa inawezekana.
“Kauli mbiu hii inalenga kutoa msukumo wa utekelezaji wa mikakati mbalimbali ya kudhibiti UKIMWI kitaifa na kimataifa ili kufikia azma ya sifuri tatu zinazomaanisha maambukizi mapya sifuri, vifo vitokanavyo na UKIMWI sifuri na unyanyapaa sifuri ifikapo mwaka 2018”.
Kauli mbiu hii pia inahimiza utekelezaji wa dhati wa malengo ya Maendeleo ya Milenia na maazimio yaliyowekwa kwenye mkutano maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu UKIMWI uliofanyika mwaka 2001 nchini Marekani”, alisema Dkt. Mrisho.
Amesema kipaumbele cha maadhimisho ya mwaka huu ni upimaji wa hiari wa VVU na ushauri nasaha, na kutoa  wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi ili wapate huduma hii muhimu.
Aidha Mkurugenzi huyo amewataka wananchi kuadhimisha siku hiyo kwa njia ya makongamano, kumbukumbu za waliofariki kwa UKIMWI, midahalo, mikutano ya wazi, vipindi kupitia vyombo vya habari, kutembelea na kutoa misaada kwa watoto yatima na wanaougua ugonjwa huo  na kutoa elimu inayohusu kujikinga na maambukizi.
Akizungumzia kuhusu upatikanaji wa dawa za kupunguza makali ya ugonjwa wa UKIMWI Mkurugenzi wa Sera, Mipango na Utafiti wa TACAIDS Dkt. Raphael Kalinga amesema dawa hizo hutolewa  bila malipo kwa wahitaji wanaostahili kuzipata hii ni kulingana na mfumo wa utoaji kwa wahitaji.
Na Beatrice Lyimo na Aron Msigwa- MAELEZO

KAMPUNI ZA ASAS ZAONGOZA KWA ULIPAJI KODI BORA KWA MKOA WA IRINGA

Mkurugenzi  wa makampuni ya  Asas  Bw  Salim Abri  Asas  kushoto akipokea cheti  maalum kutoka kwa kaimu mkuu wa mkoa wa Iringa Dr Letici Warioba  baada ya  kuibuka  mshindi wa kwanza katika  ulipaji kodi mkoa wa Iringa leo

Meneja  wa TRA mkoa wa Iringa Rosalia Mwenda akimpongeza  Bw  Asas  kwa ushindi katika ulipaji kodi
Cheti  kilichotolewa kwa  kampuni ya Asas
Salim Asas  akionyesha  cheti kwa wanahabari  baada ya  kukabidhiwa  cheti  hicho kwa kuwa mlipaji  kodi mzuri
Mzee Kaundama  akipokea  cheti
Meneja  wa TRA  Iringa Bi Mwenda akitoa maelezo ya  awali
Meza  kuu
Wanafunzi  wakiigiza  igizo la matumizi ya mashine ya EFDS
Wadau wa TRA  Iringa  wakiwa katika sherehe ya siku ya mlipa kodi
Baadhi ya  waalikwa wakishuhudia

DIAMOND AACHIA NYIMBO MPYA, NTAMPATA WAPI?BOFYA HAPA UJIONEE VIDEO YAKE.

Monday, November 17, 2014

WADAU WA FILAMU WAKUTANA NA KUJADILI MAENDELEO YA TASNIA YA FILAMU NCHINI.

 Katibu Bodi ya Filamu Tanzania, Bi. Joyce Fissoo (kulia) akieleza jambo wakati wa mkutano wa kujadili mambo yanayohusu tasnia ya filamu Tanzania uliofanyika leo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Afisa wa Bodi hiyo, Bw. Benson Mkenda.

Kaimu Mwenyekiti Bodi ya Filamu Tanzania, Sylivester Sengerema akieleza jambo wakati wa mkutano wa kujadili mambo yanayohusu tasnia ya filamu Tanzania uliofanyika katika ofisi za bodi hiyo leo jijini Dar es Salaam. 

Kaimu Mwenyekiti Bodi ya Filamu Tanzania, Sylivester Sengerema (kushoto) akieleza jambo wakati wa mkutano wa kujadili mambo yanayohusu tasnia ya filamu Tanzania uliofanyika katika ofisi za bodi hiyo leo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mjumbe wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF), Bw. John Lister
 Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF), Bw. Simon Mwakifwamba akichangia mada katika mkutano uliohusu masuala ya tasnia ya filamu Tanzania uliofanyika leo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Makamu wa Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF), Bw. Deosonga Njelekela.
Wadau kutoka Bodi ya Filamu Tanzania pamoja na Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) wakimsikiliza Katibu wa TAFF (hayupo pichani) wakati alipokuwa akichangia mada kuhusu masuala ya filamu nchini wakati wa mkutano uliofanyika katika Ofisi za Bodi ya Filamu jijini Dar es Salaam.
Katibu wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF), Bishop Hiluka akichangia mada katika mkutano uliohusu masuala ya tasnia ya filamu Tanzania uliofanyika katika ofisi za bodi ya Filamu Tanzania leo jijini Dar es Salaam.
(PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA-MAELEZO-DSM)
 

Wednesday, July 23, 2014

WAUMINI WA DINI YA KIISLAM NA WANANCHI WA PEMBA WAMSHUKURU RAIS KIKWETE KWA KUWAANDALIA FUTARI IKURU YA WETE.

 Baadhi ya waumini wa dini ya Kiislamu pamoja na wananchi wa Mikoa miwili ya Pemba wakifutari pamoja hapo ikulu ya Wete futari iliyoandaliwa na
Rais wa Jamuhuri ya Mauungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete akawakilishwa kwa niaba ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar ,h. Mohd Aboud Mohd kati kati akiwa pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Mh. Dadi Faki Dadi kulia kwake na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kaskazini Pemba Mzee Mberwa Hamad Mberwa wakijumuika na wananachi wa mikoa miwili ya Pemba kwenye futari iliyoandaliwa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete.








Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akitoa shukrani kwa niaba ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Kikwete mara baada ya futari ya pamoja kwa wananchi wa mikoa miwili ya Pemba.
Balozi Seif akiwaaga na baadhi ya wananchi wa mikoa miwili ya pemba waliohudhuria futari ya pamoja iliyoandaliwa na Rais Kikwete hapo Ikulu ya Wete
Pemba.
Balozi Seif akibadilishana mawazo na
 mmoja wa watoto walioshiriki futari ya pamoja iliyoandaliwa na Dr. Mrisho Kikwete hapo wete Pemba.
Picha na Hassan Issa wa – OMPR – ZNZ.

Press  Release:-
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amewahimiza Waumini wa Dini ya Kiislamu Nchini kuendelea kushikamana kwa lengo la kutekeleza maamrisho ya dini yao kama inavyoagiza wakati wote.Balozi Seif alitoa himizo hilo kwa niaba ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete mara baada ya futari ya Pamoja iliyoandaliwa na Rais Kikwete kwa ajili ya Wananchi wa Miko miwili ya Pemba hapo katika Majengo ya Ikulu ya Serikali ya Muungano yaliyopo  Mjini Wete Pemba.
Balozi Seif alisema njia ya kusimamisha mshikamano kwa waislam hupatikana katika mjumuisho wa makundi ya ibada akiyataja kuwa ni pamoja na madrsasa, sala pamoja na
mikusanyiko ya kufutari kwa pamoja.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif alisema
 kitendo cha Rais Kikwete cha kukutanisha waumini na baadhi
 ya wananchi katika maeneo tofauti Nchini kwa ajili ya futari
ya pamoja ni moja ya njia ya kuwajengea waumini hao ushirikiano utakaoongeza mapenzi baina yao.
Balozi Seif aliwatakia funga njema pamoja na kusherehekea kwa amani na upendo siku kuu ya Idd el fitri waumini wote wa
Zanzibar .
Akitoa shukrani kwa niaba ya wananchi wa mikoa miwili ya Pemba Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Mh. Dadi Faki Dadi
alimshukuru Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr.
Jakaya Mrisho Kikwete kwa moyo wake wa kutekeleza ibada
hiyo. Mh. Dadi alisema mpango huo wa Rais Kikwete ambao pia hufanywa ba baadhi ya Viongozi wa wengine wa juu hapa
nchini, wakiwemo pia wale wa Taasisi za umma na binafsi
hutoa faraja kwa waumini ambao hali yao ya kipato ni duni
katika kujipatia futari.

 Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
Press  Release:-
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amewahimiza Waumini wa Dini ya Kiislamu Nchini kuendelea kushikamana kwa lengo la kutekeleza maamrisho ya dini yao kama inavyoagiza wakati wote.
Balozi Seif alitoa himizo hilo kwa niaba ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete mara baada ya futari ya Pamoja iliyoandaliwa na Rais Kikwete kwa ajili ya Wananchi wa Miko miwili ya Pemba hapo katika Majengo ya Ikulu ya Serikali ya Muungano yaliyopo  Mjini Wete Pemba.
Balozi Seif alisema njia ya kusimamisha mshikamano kwa waislam hupatikana katika mjumuisho wa makundi ya ibada
akiyataja kuwa ni pamoja na madrasa, sala pamoja na mikusanyiko ya kufutari kwa pamoja. Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif alisema
Kitendo cha Rais Kikwete cha kukutanisha waumini na baadhi ya wananchi katika maeneo tofauti Nchini kwa ajili ya futarivya pamoja ni moja ya njia ya kuwajengea waumini hao ushirikiano utakaoongeza mapenzi baina yao.
Balozi Seif aliwatakia funga njema pamoja na kusherehekea kwa amani na upendo siku kuu ya Idd el fitri waumini wote wa Zanzibar .
Akitoa shukrani kwa niaba ya wananchi wa mikoa miwili ya Pemba Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Mh. Dadi Faki Dadi alimshukuru Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr.Jakaya Mrisho Kikwete kwa moyo wake wa kutekeleza ibada hiyo.Mh. Dadi alisema mpango huo wa Rais Kikwete ambao pia hufanywa na baadhi ya Viongozi wa wengine wa juu hapa nchini, wakiwemo pia wale wa Taasisi za umma na binafsi hutoa faraja kwa waumini ambao hali yao ya kipato ni duni katika kujipatia futari.

Othman Khamis Ame. Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar

Thursday, July 3, 2014

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL, AFANYA MAZUNGUMZO NA RAIS WA BURUNDI MJINI BUJUMBURA

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Rais wa Burundi Mhe. P. Nkurunziza alipomtembelea Ofisini kwake Ikulu jijini Bujumbura jana Julai 02-2014.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na waandishi wa Habari wa Vyombo mbalimbali vya Burundi Ikulu jijini Bujumbura jana ambapo alizungumzia kuhusu kuimarisha ushirikiano kati ya Nchi mbili hizi.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na baadhi ya  Viongozi wa Serikali ya Burundi kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Bujumbura jana baada ya kuhudhuria maadhimisho ya miaka 52 ya Uhuru wa nchi hiyo. Picha na OMR
*************************************
MAKAMU WA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA AFANYA MAZUNGUMZO NA RAIS WA BURUNDI, MHESHIMIWA PIERRE NKURUNZINZA
Julai 02, 2014: Bujumbura
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal, leo Jumatano Julai Pili, 2014 amekutana na Rais wa Burundi Mheshimiwa Pierre Nkurunzinza na kufanya naye mazungumzo. Mazungumzo hayo yamefanyika katika Ofisi ya Rais Nkurunzinza iliyopo katikati ya jiji la Bujumbura.
Katika mazungumzo hayo, viongozi hao walipata fursa ya kubadilishana mawazo kuhusu uhusiano baina ya Tanzania na Burundi ambapo Mheshimiwa Makamu wa Rais alitumia nafasi hiyo kumpongeza Rais Nkurunzinza na watu wa Burundi kwa sherehe zilizofana za kutimiza miaka 52 ya uhuru. Pia alitumia nafasi hiyo kumtakia kila la heri Mheshimiwa Rais Nkurunzinza pamoja na  watu wa Burundi kufuatia kupiga hatua kubwa za kimaendeleo sambamba na kuweza kuwafanya wananchi wa Burundi kuwa wamoja.
Pia alimueleza Rais Nkurunzinza kuhusu umuhimu wa kuzidi kuifanya Burundi kuwa nchi moja kwa kuwaunganisha watu wake na akaeleza kuwa, Tanzania inafurahi kuona hatua kubwa za kimaendeleo zikipigwa nchini Burundi na kwamba ili hatua hizo ziwe madhubuti, upo umuhimu wa kuwafanya wananchi wa Burundi kubakia wamoja na wanaoshirikiana katika kuiendeleza nchi yao.
“Burundi ikifanya vizuri maana yake ni kuwa Afrika Mashariki imefanya vizuri. Tanzania tutafurahi na nchi zote za ukanda wetu zitafurahi,” alisema Mheshimiwa Makamu wa Rais na kuongeza kuwa lengo la Tanzania siku zote ni kuona jirani zake wakiishi kwa utulivu na wakifanya mambo yao ya maendeleo katika hali ya amani.
Katika mazungumzo hayo Rais Nkurunzinza aliendelea kuishukuru Tanzania kwa uhusiano wake wa karibu na Burundi na akaongeza kuwa wananchi wa nchi yake wamefurahishwa sana kwa Tanzania kushiriki katika sherehe za miaka 52 ya Uhuru wa Burundi, sherehe zilizofanyika katika Uwanja wa Prince Louis Rwagasore jana. Pamoja na Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Tanzania, sherehe hizo pia zilihudhuriwa na Makamu wa Rais wa Somalia na Waziri Mkuu wa Chad.
Msafara wa Mheshimiwa Makamu wa Rais umeondoka leo jijini Bujumbura na kurejea jijini Dar es Salaam tayari kabisa kuendelea na majukumu mengine ya kitaifa. Katika msafara huo, Mheshimiwa Makamu wa Rais aliambatana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Zanzibar, Mheshimiwa Haroun Ali Suleiman na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mheshimiwa Mahadhi Juma Maalim.
Imetolewa na:              Ofisi ya Makamu wa Rais
Julai 2, 2014 Bujumbura: Burundi

Friday, June 27, 2014

MTEMVU: WAPINZANI HATA WAKIUNGANA VIPI CCM ITAWABWAGA, ASHANGAA KUAMBIWA ANA MASLAHI BINAFSI KUWATETEA MAMALISHE

 Mbunge wa Temeke, Abbas Mtemvu akifungua Kikao cha Baraza Kuu la Jumuia ya Wazazi ya CCM, wilaya ya Temeke, leo katika ukumbi wa Manispaa ya wilaya hiyo jijini Dar es Salaam.
 Mbunge wa Temeke, Abbas Mtemvu ambaye pia ni Mjumbe wa NEC, akimkabidhi hati ya pongezi , Zaitun Lukinga, ya kuwa kiongozi wa Jumuia ya Wazazi awamu zaidi ya moja katika nafasi ya Katibu wa Jumuia ya wazazi Kata ya Kurasini, wakati wa mkutano huo leo
 Washiriki wakiwa kwenye mkutano huo. Habari Picha na Bashir Nkoromo-
Jun 27, 2014

NA BASHIR NKOROMO, TEMEKE
MBUNGE wa Temeke Abbas Mtemvu amewananga wapinzani akisema hata wakisimamisha mgombea mmoja mmoja, katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2015, CCM itawabwaga.
Amesema, uhakika huo anao na hata wapinzani wenyewe wanajua hilo, kwa kuwa hawaizidi CCM kwa weledi wa kisiasa, kwa akili wala wingi wa wanachama.
Mtemvu amsema hayo wakati akifungua kikao cha Baraza Kuu la Jumuia ya Wazazi Wilaya ya Temeke, kilichofanyika leo, Juni 27, 2014, kwenye Ukumbi wa Manispaa ya wilaya hiyo, mjini Dar es Salaam.
"Wapinzani baada ya kuona kuwa hawatuwezi kwa kila chama kivyake, sasa mnaona wanavyotapatapa, mara eti huo Ukawa walioanzisha wanataka pia kuutumia kwenye chaguzi, kuweka mgombea mmoja mmoja kwa wote, mimi bado naamini hata wafanyeje CCM itawabwaga tu", alisema Mtemvu.
Mtemvu alisema, pale ambapo wapinzani wamekuwa wakipenya na kunyakuwa ubunge au udiwani ni pale ambapo CCM wenyewe wanakuwa wamejichanganya.
"Ikifika acheni mambo ya kuanza mizozano ya ndani kwa ndani kutokana na makundi ambayo husababishwa na baadhi ya wagombea au wanachama wanaowataka wagombea kwa lazima, tukiachana na hili nawahawakikhieni wapinzani hawapati hata kiti kimoja cha cha mtaa", alisema Mtemvu.Mtemvu aliwataka wana-CCM pia kuachana na mambo ya kushughulika tu na wanaotaka nafasi ambao wana fedha, akisema, kufanya hivyo kunasababisha baadhi kuwa wagombea kutokana na uwezo wa fedha tu na siyo wa uongozi.
Aliwataka mtu anapowajia kwa fedha kuzipokea na kuzila, lakini wakati waanapofikia maamuzi muhimu kwenye uchaguzi wahakikishe wanachagua yule wanayemfahamu kwa thati kwamba anao uwezo wa uongozi.
Alisema, wapo baadhi ya wanachama wa CCM wanao uwezo wa kuongoza lakini hawana fedha, hivyo watu wa aina hiyo wasitoswe kwa sababu ya ufukara wao.

Mtemvu alisema kiongozi mwenye uwezo ni yule anayekubalika na watu, saa zote yupo na watu na anajali maslahi ya wanyonge siyo wale anaowajua kuwa ni wake tu.



"Mfano ni kama hivi tunavyofanya sasa wabunge wa mkoa wa Dar es Salaam. Kila mara tunapigania wanyonge, juzi nimepambana kuwatetea mamalishe wasifukuzwe hovyo, japo baadhi ya watu tena waliopewa malmaka na Rais waknibeza eti nina maslahi binafsi, khaa, yaani mimi niwe na maslahi na mamalishe huu kama siyo uzushi ni nini?" alisema Mtevu. 

U.S. EMBASSY DAR ES SALAAM CELEBRATES THE 238th ANNIVERSARY OF AMERICAN INDEPENDENCE.

United States Ambassador to Tanzania Mark B. Childress (left) and Tanzania’s Minister for Natural Resources and Tourism Lazaro Nyalandu toastthe 238th anniversary of American Independence and the bonds of friendship between the two countries.  Minister Nyalandu joined scores of Tanzanians, members of the diplomatic corps, and other distinguished guests at a colorful Independence Day reception at the U.S. Embassy in Dar es Salaam on June 26, 2014. (Photo courtesy of the American Embassy)

        U.S. Embassy Tanzania
                    Press Release

June 27, 2014
U.S. Embassy Dar es Salaam Celebrates the
238th Anniversary of American Independence
In celebration of the 238th anniversary of American Independence, United States Ambassador to Tanzania Mark Childress hosted a colorful reception at the U.S. Embassy grounds on June 26 in Dar es Salaam.  The event focused on four iconic cities in the U.S.: Boston, Los Angeles, Chicago and New Orleans, and finished off with a fireworks display.  The guest of honor from the Government of Tanzania was Hon. Lazaro Nyalandu, Minister for Natural Resources and Tourism. 
Addressing an audience of approximately 500 guests, Ambassador Childress remarked that both the United States and Tanzania stand for liberty, justice and prosperity.  At his first Independence Day celebration as the U.S. Ambassador to Tanzania, Ambassador Childress pledged to further strengthen the friendship between the two nations.  More specifically, Ambassador Childress said he will work closely with the Government and People of Tanzania to address the problem of wildlife trafficking.
In his remarks, Hon. Lazaro Nyalandu congratulated the American people on the occasion of their Independence Day, and remarked on the birth of the relationship between the U.S. and Tanzania with the close friendship between the late Mwalimu Julius Nyerere and the late President John F. Kennedy.  Minister Nyalandu also commended Ambassador Childress for his commitment to wildlife conservation, and pledged to ensure Tanzania does all that is within its powers to combat the problem of elephant poaching.
The United States’ Independence Day, commonly referred to as Fourth of July, is celebrated to commemorate the adoption of the Declaration of Independence on July 4, 1776, announcing the separation of America from Great Britain.

BALOZI IDDI AFUNGUA MSIKITI WA IJUMAA WA KIJIJI CHA MAMBOLEO BAADA YA KUFANYIWA UKARABATI

  Balozi Seif akizungumza na waumini wa Dini ya Kiislamu wa Kijiji cha Kiboje Mamboleo mara baada kuufungua msikiti wao wa Ijumaa uliofanyiwa matengenezo makubwa.
Mwakilishi wa Jimbo la Uzini Mh. Moh’d Raza Hassanali akielezea mikakati ya kamati ya ujenzi wa misikiti, Madrasa na maskuli nchini ilivyopania kuendeleza malengo yake.
*********************************************
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amezikumbusha Kamati za Misikiti hapa  nchini kuendelea kuwa imara kwa kutowaruhusu watu wanaopenda kujipenyeza ndani ya kamati hizo kwa nia ya kuanza kutoa madarasa ya uchochezi na kuwagawa waumini kimadhehebu.
Alisema uimara huo ndio njia sahihi itakayoilinda misikiti hiyo na wimbi la vurugu na migogoro ambayo hatiae husababisha mmong’onyoko mkubwa wa  ukosefu wa maadili  katika jamii za kiislamu.
Akiufungua msikiti mpya wa Ijumaa uliofanyiwa matengenezo makubwa katika Kijiji cha Kiboje Mambo leo Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif alisema msikiti ni taasisi yenye mchango mkubwa wa kuutangaza ukweli dhidi ya unafiki pamoja na mambo ya kheri kwa jamii ya Kiislamu.
Balozi Seif alisema katika kuihuisha nyumba ya Mwenyezi Muungu  Msikiti ni vyema kwa waumini hao mbali ya kutekeleza vipindi vya sala lakini pia ni vyema wakaendeleza madarasa hasa kipindi hichi kinachokaribia cha  mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani kwa kujifunza masuala ya dini yao.
Alisema waumini wa dini ya  Kiislamu wanaotekeleza ibada zao na kusimamisha sala katika vipindi vitano kwa siku hupata baraka na neema ya kuwa wageni wa mola wao aliyewaumba.
“ Nani miongoni mwetu hataki kuwa mgeni wa mola wake mara tano ? Kama jawabu ni ndio basi tuhakikishe tunaswali mara tano kama tulivyoamrishwa na mola wetu. Na zile Baraza la manzese zisiwepo tena hapa mtaani penu“. Alisisitiza Balozi Seif.   
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliwanasihi wananchi wa maeneo hayo hasa vijana kuachana na maasi ya unywaji pombe kiholela ambayo huchangia vitendo vya wizi wa mazao na mifugo katika maeneo mbali mbali nchini.
Alisema hivi sasa jamii imekuwa ikishuhudia mmong’onyoko mkubwa wa utamaduni wa Kiislamu na kupelekea kuibuka kwa vitendo vya ubakaji na unyanyasaji wa watoto na wanawake kijinsia.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliwanasihi watu wenye kupenda kunywa pombe kuachana na tabia hiyo inayozototesha hata afya zao na badala yake waelekeze  juhudi zao katika kilimo cha mazao ya biashara na chakula kwa lengo la kujijengea hatma njema ya baadaye.
Aliipongeza Kamati ya uendelezaji wa ujenzi wa misikiti, madrasa na maskuli Nchini kwa uamuzi wake wa kuufanyia matengenezo makubwa msikiti huo wa Kiboje Mamboleo ambao ulikuwa katika hali mbaya.
Balozi Seif alielezea imani yake kwamba waumini wa msikiti huo wataendelea kuutunza na kujiepusha na migogoro ya kugombania uongozi ambao hatiae huzaa chuki na hasama zisizo kwisha kwa kipindi kirefu.
“ Misikiti sio sehemu ya kutangazwa sera za siasa kama Viongozi na wahutubu katika baadhi ya misikiti kupendelea kukashifu viongozi waliopo madarakani  wakati kinachowapeleka  kwenye nyumba hiyo tukufu ni kufanya ibada pekee “. Alifafanua Balozi Seif.
Aliwataka na kuwahimiza waumini hao pamoja na wananchi wa maeneo hayo kuwakataa na kuwatenga watu wote waliojikubalisha kubeba cheche ya shari na utenganifu ndani ya jamii.
Akisoma risala ya waumini na wananchi hao wa Kiboje Mamboleo Ustadhi Juma Abdulla alisema wana jamii hao wameelezea faraja yao kutokana na kumalizika kwa ujenzi wa msikiti huo.
Ustadhi Juma Abdulla hata  hivyo alisema bado zipo baadhi ya changa moto zinazoendelea kuwakabili wana jamii hao wa Kiboje Mambo leo ambazo zimekuwa zikiwapa wakati mgumu kwao na kizazi chao.
Alizitaja baadhi ya changamoto hizo Ustadhi Juma alisema kuwa ni pamoja na madrasa, eneo la michezo ya watoto wa kiislamu hasa wakati wa siku kuu pamoja na matengenezo ya chuo cha Qurani kilichopo jirani na msikiti huo.
Mapema Mwenyekiti wa Kamati ya usimamizi wa ujenzi wa Misikiti, madrasa na majengo ya skuli hapa Zanzibar ambae pia ni Mwakilishi wa Jimbo la Uzini Mh. Moh’d Raza Hassanali alisema kamati hiyo iliyo chini ya mwenyekiti wake Rais Mstaafu wa Tanzania Alhajj Ali Hassan Mwinyi itaendelea kuongeza nguvu zake kwenye ujenzi wa majengo ya taasisi hizo yenye upungufu hapa Nchini.
Mh. Raza aliwahakikishia wana jamii hao wa Kiboje Mamboleo  kwamba uongozi wa Jimbo hilo uko katika jitihada za makusudi katika kukabiliana na changamoto zinazowakabili wana jamii hao ikiwemo ya ubovu wa bara bara.
Msikiti wa Kijiji cha Kiboje Mamboleo uliofanyiwa matengenezo makubwa hivi sasa una uwezo wa kusaliwa sala ya kawaida au ile ya Ijumaa na waumini wasiopunguwa mia tatu.