Monday, August 20, 2012

Full Yanga 4-African Lyon 0, Msuva ang'ara


Kiungo mshambuliaji wa timu ya Yanga, Haruna Niyonzima (kulia) akimsakata kiungo wa  African Lyon, wakati wa mchezo wa kirafiki wa kujiandaa na Ligi Kuu Tanzania Bara, inayotarajia kuanza hivi karibuni, uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, leo jioni. Katika mchezo huo Yanga imeibuka na ushindi wa Mabao 4-0. Bao la kwanza la Yanga, limefungwa na kipa wa African Lyon, Juma Abdul, aliyejifunga katika dakika 8, kipindi cha kwanza, bao la pili limefungwa na Haruna Niyonzima kwa mkwaju wa penati, dakika ya 54, baada ya beki wa Lyon Semi Kessy, kumchezea rafu, Msuva katika eneo la hatari. Goli la tatu limefungwa na Simon Msuva, katika dakika ya 72, kufuatia pasi safi ya Frank Dumayo na bao la nne limefungwa na Jerry Tegete katika dakika ya 90+2, baada ya pasi safi ya Idrisa Rashid.
 Replay ya Penati iliyosababishwa na Simon Msuva (kushoto) akimsakata Beki wa African Lyon, Semi Kessy.
 Msuva, kapita, beki kazidiwa kaanza jitihada za ziada kumzuia kwa mkono.......
 Bado haitoshi aliona anazidi kuzidiwa, ikabidi atumie mkono na miguu kwa kumtega kwa nyuma.....
 Akaona isiwe tabu Heri lawama kuliko Fedheha.......akamaliza kazi ndani ya eneo la hatari la penati Boksi.....
 Mwamuzi wa mchezo huo akaamuru penati, hapa kipa wa African Lyon, akatoka kabla ya kupigwa mkwaju huo na Niyonzima na kupangua, mwamuzi huyo akaamuru irudiwe penati hiyo......
 Iliporudiwa, kipa huyu aliteswa kama hivi, Mpira kulia kwake yeye kushoto kwake.........Goooooooo!!!!! la tatu.
Goli lililoonekana kuzua utata kama inavyoonekana beki wa Lyon, akiokolea nyuma ya mstari....
Kocha wa timu ya Africa Lyon, Muargentina,  Pablo  Velez, akionekana kulalamikia jambo kwenye benchi la ufundi la timu yake  wakati timu yake ilipokutana na timu ya Yanga katika mchezo wa kirafiki kwenye uwanja wa Taifa jioni hii.
Kikosi cha timu ya Africa Lyon.
Kikosi cha timu ya Yanga. 

No comments:

Post a Comment