Kiungo
mshambuliaji wa timu ya Yanga, Haruna Niyonzima (kulia) akimsakata
kiungo wa African Lyon, wakati wa mchezo wa kirafiki wa kujiandaa na
Ligi Kuu Tanzania Bara, inayotarajia kuanza hivi karibuni, uliochezwa
kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, leo jioni. Katika mchezo
huo Yanga imeibuka na ushindi wa Mabao 4-0. Bao la kwanza la Yanga,
limefungwa na kipa wa African Lyon, Juma Abdul, aliyejifunga katika
dakika 8, kipindi cha kwanza, bao la pili limefungwa na Haruna
Niyonzima kwa mkwaju wa penati, dakika ya 54, baada ya beki wa Lyon
Semi Kessy, kumchezea rafu, Msuva katika eneo la hatari. Goli la tatu
limefungwa na Simon Msuva, katika dakika ya 72, kufuatia pasi safi ya
Frank Dumayo na bao la nne limefungwa na Jerry Tegete katika dakika ya
90+2, baada ya pasi safi ya Idrisa Rashid.
Replay ya Penati iliyosababishwa na Simon Msuva (kushoto) akimsakata Beki wa African Lyon, Semi Kessy.
Msuva, kapita, beki kazidiwa kaanza jitihada za ziada kumzuia kwa mkono.......
Bado haitoshi aliona anazidi kuzidiwa, ikabidi atumie mkono na miguu kwa kumtega kwa nyuma.....
Akaona isiwe tabu Heri lawama kuliko Fedheha.......akamaliza kazi ndani ya eneo la hatari la penati Boksi.....
Mwamuzi
wa mchezo huo akaamuru penati, hapa kipa wa African Lyon, akatoka kabla
ya kupigwa mkwaju huo na Niyonzima na kupangua, mwamuzi huyo akaamuru
irudiwe penati hiyo......
Iliporudiwa, kipa huyu aliteswa kama hivi, Mpira kulia kwake yeye kushoto kwake.........Goooooooo!!!!! la tatu.
Goli lililoonekana kuzua utata kama inavyoonekana beki wa Lyon, akiokolea nyuma ya mstari....
Kocha
wa timu ya Africa Lyon, Muargentina, Pablo Velez, akionekana
kulalamikia jambo kwenye benchi la ufundi la timu yake wakati timu
yake ilipokutana na timu ya Yanga katika mchezo wa kirafiki kwenye
uwanja wa Taifa jioni hii.
Kikosi cha timu ya Africa Lyon.
Kikosi cha timu ya Yanga.