Monday, July 1, 2013

*OBAMA ATUA BONGO, APOKELEWA KWA MUZIKI NA MATARUMBETA ASEBENEKA KWEUPEEEEEE


Rais Jakaya Kikwete, akiwa na mgeni wake, Rais wa Marekani, Barack Obama, baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam, leo mchana huku kwa pamoja wakifurahia na kucheza ala za muziki wa Matarumbeta uwanjani hapo. 
Baada ya kuwasili Uwanjani hapo Obama, alikagua Gwaride maalum na kusalimiana na wananchi waliokusanyika uwanjani hapo kwa kuwapungia mikono, ambapo aliwaacha hoi wananchi hao pale alipofika mbele ya wasanii wa muzuki wa matarumbeta na kuanza kusebenekwa kwa kucheza muziki huo huku akishangiliwa na umati mkubwa wa watu. 
Baada ya hapo Obama na msafara wake walielekea Ikulu ambapo pia alikuwa na kikao cha faragha na mwenyeji wake na baadaye kuzungumza na waandishi wa habari, walioruhusiwa kuuliza maswali na kujibiwa papo hapo.
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Rais Barrack Obama wa Marekani muda mfupi baada ya kuwasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam mchana wa leo. Kulia ni Mke wa Rais Mama Salma Kikwete.
 Rais Barack Obama na Familia yake wakishuka kutoka ndege ya Airforce One muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam leo mchana.
 Rais Barack Obama na Familia yake wakishuka kutoka ndege ya Airforce One muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam leo mchana.
 Hawa ni baadhi ya wananchi waliojitokeza pande za Barabara mpya ya Obama, geti kubwa la Ikulu kwa ajili ya kumlaki Rais Obama.
 Wakimsubiri Obama.....
 Hawa pia ni baadhi tu ya wananchi walikuwa katika njia za makutano ya Barabara aliyopita Obama, wakisubiri kumlaki.
 Njia zote zilizo katika makutano na barabara aliyopita Obama zilifungwa kwa muda kama hivi. PICHA NA KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPO CHINI

No comments:

Post a Comment