Tuesday, July 2, 2013

*RAIS OBAMA NA UJUMBE WAKE WAMEONDOKA LEO


 Rais wa Marekani, Barack Obama na mkewe Michelle, wakipanda ndege yao aina ya Air Force One, tayari kuondoka nchini kurejea nchini kwao baada ya kumaliza rasmi ziara yao katika Bara la Afrika, ambapo amemalizia ziara hiyo kwa kufanya ziara ya siku mbili nchini Tanzania. Obama na msafala wake ameondoka leo mchana.
 Rais Obama na mkewe, wakipunga mikono kuwaaga wenyeji wao Rais Jakaya Kikwete na mkewe, Viongozi wa Kiserikali na wananchi waliofika uwanjani hapo kuwaaga leo, mchana wakati wakiondoka nchini.
 Rais Jakaya Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete, wakipunga mikono kuwaga wageni wao Rais Obama na mkewe wakati wakiondoka nchini leo mcahana baada ya kumaliza ziara yao.
 Rais Barack Obama akiagana na Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es salaam huku Mstahiki Meya wa Ilala pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Liberata Mulamula wakisubiri zamu zao.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Barack Obama wakipokea saluti wakati nyimbo za Taifa zikipigwa wakati wa kuondoka kwa Rais huyo wa Marekani leo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere. Nyuma yao ni Mama Salma Kikwete na Mama Michelle Obama pamoja na Mkuu wa majeshi Jenerali Davis Mwamunyange pamoja na IGP Saidi Mwema . Kushoto ni Mkuu wa Itifaki Balozi Mohamed Maharage na Mkuu wa Itifaki wa Ikulu ya Marekani (White House) Balozi Capricia Marshall. Ziara ya Rais Obama nchini imetajwa kuwa moja ya ziara za viongozi wa nje zilizofanikiwa sana, ambapo maelfu ya Watanzania walijitokeza kumlaki na kumuaga.

No comments:

Post a Comment