Saturday, March 29, 2014

*CHEKI VIDEO MPYA YA WAKONGWE, PROF, JAY, J. NATURE NA JAY MOE, WAMETISHA NA GWANDA ZA KIJEDA



Na Dina Ismail, Dar es Salaam
WASANII watatu wakongwe na maarufu wa muziki wa Bongo Fleva nchini, Juma Mchopanga ‘Jay Moe’, Juma Kassim ‘Nature’ na Joseph Haule ‘Profesa Jay’ wamerekodi kwa pamoja wimbo mpya uitwao JWTZ ikiwa ni pamoja na video yake hii.
Sauti ya wimbo huo na Video umerekodiwa katika studio za Williamz Visions chini ya mtayarishaji Mike Mwakatundu ‘Mike T’. 
Akizungumza na mwandishi wa habari hii, mtayarishaji huyo, Mike T, maarufu kama Mnyalu, amesema kuwa, yeye anakuwa muongozaji wa kwanza wa video au filamu Tanzania kupata fursa ya kutumia vifaru, ndege, helikopta na sare za Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) katika kazi zake.

“Naamini kwa kumtanguliza Mungu kila kitu kinawezekana, baada ya yote, naamini magwiji hao wamefunika katika video  hii na wamefanya kweli,”amesema Mike T, ambaye pia ni gwiji wa Bongo Fleva.

No comments:

Post a Comment