Sunday, March 30, 2014

FAINALI ZA KLABU BINGWA AfFRIKA MASHARIKI KWA MCHEZO WA NETIBOLI WAMALIZIKA

 Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Bw Leonard Thadeo akisalimiana na wachezaji wa Timu ya Shirika la Taifa la Bima (NIC) Uganda wakati  wa  fainali  ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki kwa mchezo wa Netiboli ambayo walicheza na JKT Mbweni  ya Tanzania jana jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi wa Maendeleo ya  Michezo Bw Leonard Thadeo akimkabidhi Kombe  la mshindi     wa kwanza wa mashindano  ya netiboli  Klabu  Bingwa Afrika Mashariki nahodha wa Timu ya NIC Uganda  Obua Desire, baada ya kuifunga timu ya JKT Mbweni ya Tanzania magoli 47–30 jana jijini Dar es Salaam.

 Wachezaji wa timu ya NIC Uganda wakifurahia ushindi  uliopelekea kutetea ubingwa wajana jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Chama cha mpira wa Netiboli Tanzania ( Chaneta ) Bi. Anna Kibira 9kusoto) -akikabidhiwa majukumu ya Shirikisho la vyama vya mpira wa netiboli Afrika Mashariki (EANA) na Rais   wa Shirikisho hilo Bi.Mildred Ajiemba Wanyama jana jijini Dar es Salaam. Tanzania imekabidhi kuongoza sekretariati ya shirikisho hilo kutoka nchi ya Kenya.
              Picha zote  na FrankShija Afisa Mawasiliano Serikalini WHVUM.

No comments:

Post a Comment