Tuesday, March 25, 2014

*RAIS KIKWETE AZINDUA UKARABATI WA BARABARA YA KOROGWE HADI MKUMBARA

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete(wapili kushoto),Wziri wa Ujenzi Dkt.John Magufuli(kushoto), Mkurugenzi wa Benki ya Dunia kwa nchi za Tanzania,Burundi na Uganda Bwana Philippe Dongier(watatu kushoto),Mwakilkishi wa Kampuni ya ujenzi ya Strabag Bwana Philip Raiver(wanne kushoto) na mkurugenzi Mtendaji wa TANROADS mhandisi Patrick Mfugale(kulia) wakiata utepe kuzindua rasmi uakarabati wa Barabara ya Korogwe-Mkumbara yenye urefu wa kilometa 76 jana mjini Korogwe.Ukarabati huo unafadhiliwa na Benki ya Dunia.
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete(katikati), Waziri wa Ujenzi Dkt.John Pombe Magufuli(kushoto), pamoja na Mwakiklishi wa Benki ya Dunia Bwana Philippe Dongier wakifunua kitambaa katika jiwe la msingi kuashiria kuzindua rasmi ukarabati wa barabara ya Korogwe hadi Mkumbara kwa ufadhili ya Benki ya dunia.Uzinduzi huo ulifanyika mjini Korogwe jana .Wanne kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga Lutemi Mstaafu Chiku Galawa.
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiandaa kuapanda mti wa kumbukumbu wakati wa hafla ya uzinduzi wa ukarabati wa Barabara ya Korogwe hadi Mkumbara jana mjini Korogwe huku mwakilkishi wa Benki ya Dunia inayofadhili mradi huo Bwana Phillippe Dongier akiangalia. 
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiteta jambo na Mkurugenzi wa Benki ya Dunia kata ya nchi za Tanzania, Burundi na Uganda Bwana Philippe Dongier (kushoto) wakati wa hafla ya uzinduzi wa ukarabati wa Barabara ya Korogwe Mkumbara yenye urefu wa kilometa 76 uliofanyika jana mjini Korogwe.Kulia ni Waziri wa ujenzi Mh. John Pombe Magufuli. Picha na Freddy Maro.

No comments:

Post a Comment