Sunday, March 30, 2014

*TAMASHA LA MUZIKI KUHUSU MUUNGANO LAFANA


 Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Pro. Elisante Ole Gabriel akifungua Tamasha la Muungano la Fainali la Muziki wa Dansi, Taharabu, Kizazi Kipya na Utenzi siku ya Jumamosi katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
 Mgeni rasmi katika Tamasha la Muungano la Fainali la Muziki wa Dansi, Taharabu, Kizazi Kipya na Utenzi Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Bi. Regina Kikuli akitoa hotuba fupi wakati wa tamasha hilo, kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Pro. Elisante Ole Gabriel.
 Mshereheshaji kutoka kikundi cha Temeke akionyesha umahiri wake kwa  kula moto wakati wa Tamasha la Muungano la Fainali la Muziki wa Dansi, Taharabu, Kizazi Kipya na Utenzi lililofanyika siku ya Jumamosi katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

 Kundi la muziki wa dansi lijulikanalo kwa jina la Mashujaa wakitumbuiza wakati wa Tamasha la Muungano la Fainali la Muziki wa Dansi,Taharabu, Kizazi Kipya na Utenzi siku ya Jumamosi katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

Viongozi wa makundi ya muziki wa Dansi,Taarabu,Kizazi kipya na Utenzi walioshiriki Tamasha la Muungano la Fainali la Muziki wa Dansi, Taarabu, Kizazi Kipya na Utenzi wakiwa katika picha ya pamoja ambapo katika muziki wa dansi kundi la Msondo ngoma liliibuka kidedea huku upande wa taarabu Jahazi Modern Taarabu walishika nafasi ya kwanza huku muziki wa kizazi kipya msanii Kelvin Nyoni kawabwaga wenzake na katika fani ya Utenzi Bi. Mariam Mponda kashika nafasi ya kwanza.Picha na Genofeva Matemu – Afisa Mawasiliano Serikalini WHVUM

No comments:

Post a Comment