Tuesday, March 25, 2014

*MAJINA WA VIONGOZI WA KAMATI 12 ZA BUNGE MAALUM LA KATIBA NA KAMATI YA UONGOZI YATAJWA


Na Magreth Kinabo,  MaelezoDodoma   
Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba,Mhe. Samwel Sitta leo, ametangaza majina ya wenyeviti na makamu wenyeviti wa Kamati za bunge hilo.

Majina hayo yametangazwa na Mwenyekiti huyo  baada ya uchaguzi wa viiongozi hao uliofanyika (jana) Machi 24 , mwaka  2014 mjini  Dodoma .

Mwenyekiti huyo aliyataja majina hayo  katika  Kamati  ya Uandishi Mwenyekiti Andrew Chenge, Makamu wake ni Mgeni Hassan Juma. Kamati ya Kanuni Mwenyekiti ni Pandu Ameri Kificho, Makamu wake ni Dkt. Susan Kolimba. Kamati Na. 1 Mwenyekiti ni  Ummy Ally Mwalimu, na Makamu wake ni Prof. Makame  Mbalawa.

Wengine waliochaguliwa  katika Kamati Na. 2 Mwenyekiti ni Shamsi Vuai Nahodha, Makamu wake ni Shamsa Mwangunga.Kamati Na. 3 Mwenyekiti  ni  Dkt. Francis Michael, Makamu wake ni Fatma MussaJuma.

Mhe. Sitta alisema waliochaguliwa katika Kamati Na. 4 Mwenyekiti ni  Christopher  Ole-Sendeka, Makamu wake ni  Dkt. Sira Ubwa Mamboya, Kamati Na. 5 Mwenyekiti ni  Hamad Rashid Mohamed Makamu wake ni  Assumpter  Mshama.

          Viongozi waliochaguliwa katika Kamati Na. 6 Mwenyekiti Stephen Wassira na Makamu wake ni Dkt. Maua  Daftari.Kamati Na. 7  Mwenyekiti  Brig. Hassan Ngwilizi  ,Makamu wake  Waride   BakariJabu.Kamati Na. 8 Mwenyekiti  ni Job Ndugai,Makamu wake ni Biubwa Yahya   Othman.

Kamati Na. 9 Mwenyekiti ni Kidawa Hamidi Saleh,Makamu wake Wiliam  Ngeleja,Kamati Na. 10 Mwenyekiti ni Anna  Abdallah, Makamu wake ni   Salmin Awadh Salmin.Kamati Na. 11 Mwenyekiti ni Anne  Malecela, Makamu wake  Hamad  Masauni na Kamati Na. 12 Mwenyekiti  Paul Kimiti na Makamu wake ni  Thuwaybah E. Kisasi.

Wakati huohuo , Sitta  alitangaza wajumbe wa Kamati ya  Uongozi ya Bunge Maalum la Katiba, ambao  ni wenyekiti na makamu wenyeviti wa kamati hizo wakiwemo wajumbe wengine watano aliowateua.

 Wajumbe hao walioteuliwa na Sitta kuingia katika kamati hiyo ni Fakharia Khamisi Shomari, Mary Chatanda, Profesa Ibrahim Lipumba, Amon Mpanju na Hamad Abuu Juma.

 Hata hivyo pamoja na majina hayo kutangazwa Profesa Lipumba alisimama na katika nafasi hiyo 

No comments:

Post a Comment