Thursday, May 29, 2014

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AHANI MSIBA WA MKE WA KATIBU MKUU WA WIZARA YA FEDHA

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisaini kitabu cha maombolezo ya kifo cha mke wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi, Dkt. Servacius Likwelil, wakati alipofika kumfariji Katibu huyo nyumbani kwake Boko Jijini Dar es Salaam, jana jioni. Mazishi yanatarajia kufanyika leo jioni kwenye Makaburi ya Kinondoni.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akijumuika na waombolezaji katika msiba wa mke wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi,  Dkt. Servacius Likwelil, wakati alipofika kumfariji Katibu huyo nyumbani kwake Boko Jijini Dar es Salaam, jana jioni. Mazishi yanatarajia kufanyika leo jioni kwenye Makaburi ya Kinondoni. 
Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Adama Malima, akizungumza machache katika shughuli hiyo ya kuhani msiba huo.

No comments:

Post a Comment