Saturday, April 12, 2014

MAFURIKO DAR,JANGWANI,KIGOGO,MSASANI NA KWENGINEKO VILIO

Mafuriko kwa Dar es salaam nzima
Dalaja la mto mpiji lililokatika leo asubuhi limesababisha wakazi wa Bagamoyo kushindwa kufanya shughuli zao,Kukatika kwa Dalaja hilo kumesababishawakazi wa Bagamoyo kushindwa kufika Dar na wale wa Dar kutokufika Bagamoyo kutokana na kuwa ndio njia kuu. Wakazi wa Bagamoyo wakihaha baada ya kuona kwamba wameshindwa kupita katika Dalaja hilo kuendelea na majukumu yao.
Sinza nako hali ni tete soko la afrika sana nalo likiwa limezingirwa na mafuliko,kutokana na hali hii kwa wakazi wa mabondeni mnashauliwa kuondoka kwani mvua bado zinaendelea kunyesha ikiwa leo ni siku ya pili ambapoimetangazwa kunyesha kwa siku tano Mfululizo.



 Mkazi wa  jiji la Dar es Salaam  akiwa ameokoa  baadhi ya mali  zake  huku  asijue kwa kwenda  



Tanesco mmeiona hii?Mbali ya  nyumba  hizi kufunikwa na maji  ila  bado nyumba  hii  kushoto  umeme  unawaka  eneo la jangwani jambo ambalo ni hatari zaidi   (picha na Mroki Mroki)



 Hivi ndivyo  mvua  inavyowatesa  wananchi  wanaoishi mabondeni jiji  Dar es Salaam  ila bado hawataki kuhama


No comments:

Post a Comment