Thursday, May 30, 2013

*KLABU YA YANGA YAPONGEZWA NA KAMPUNI YA BIA YA KILIMANJARO LEO

Meneja wa bia ya Kilimanjaro Premium Lager, George Kavishe (kushoto) akikabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya sh. Mil. 25 kwa Katibu Mkuu wa Yanga,Laurance Mwalusako ikiwa ni sehemu ya ahadi yake kwa Timu yeyote itakayo chukua ubingwa wa Ligi Kuu.Wengine pichani ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Yanga,Mussa Katabaro,Mkurugenzi wa Fedha Yanga,Denis Oundo pamoja na Geoffrey Makau.
Meneja wa bia ya Kilimanjaro Premium Lager, George Kavishe akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) jijini Dar es Salaam leo wakati wa hafla fupi ya kuipongeza Timu ya Yanga baada ya kutwaa Kombe la Ligi Kuu Tanzania Bara,hafla hiyo imefanyika kwenye Ukumbi wa TBL Ilala Mchikichini jijini Dar es Salaam.Wengine pichani ni Katibu Mkuu wa Yanga,Laurance Mwalusako pamoja na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Yanga,Mussa Katabaro.
Katibu Mkuu wa Yanga,Laurance Mwalusako akisisitiza jambo mbele ya Waandishi wa Habari (hawapo pichani) wakati wa hafla fupi ya kuipongeza Timu ya Yanga baada ya kutwaa Kombe la Ligi Kuu Tanzania Bara.Kushoto ni Meneja wa bia ya Kilimanjaro Premium Lager, George Kavishe

No comments:

Post a Comment