Monday, May 27, 2013

*SAGA SAGA NI MAARUFU KWA KUWATOA UDENDA WASAFIRI KWA MISHIKAKI YA MBUZI


Saga saga ni eneo maarufu ambalo kwa sasa limezidi kujizolea sifa na umaarufu mkubwa kwa kuchoma nyama ya mbuzi, ambapo wasafiri wengi wanaotumia barabara kuu ya mkoa wa Morogoro kuelekea mikoa ya Iringa kabla ya kufika Kijiji cha Mbuga ya Mikumi, wamekuwa wakisimama eneo hili na kupata nyama choma kama inavyoonekanika pichani, wauzaji wakiandaa mishikaki hiyo huku baadhi ya wasafiri wakijisevia.
Mishikaki ya nyama ya mbuzi ikiandaliwa kwa ajili ya kuuzwa kwa wateja, ambapo mishikaki hiyo inauzwa kil mmoja kwa Sh. 3000. Picha na Adam Mzee

No comments:

Post a Comment