Monday, May 13, 2013

MASHUJAA BAND WAZINDUA VIDEO YAO YA RISASI KIDOLE NA FM ACADEMIA BAADA YA KUBUMA NA JB MPIANA


 Rais wa Bendi ya Fm Academia, Nyoshi El-Saadat (kushoto) akipozi na Rais wa Bendi ya Mashujaa, Charz Baba (katikati) na Makamu wa Rais wa Fm, King Braize, wakati wa shoo ya uzinduzi wa Video mpya ya Risasi Kidole ya Mashujaa, uzinduzi huo ulifanyika kwenye Ukumbi wa Green Acres, Victoria jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita. 
Nyoshi alimtunuku tuzi Charz na kumvisha ikiwa ni heshima ya kumtambua kuwa Rais wa bendi hiyo akimtakia mafanikio katika kusimamia na kuiendesha bendi hiyo kwa mafanikio. 
Mwishoni mwa maka jana bendi hiyo ilizindua albam hiyo bila mafanikio wakati ilipomualika nguli wa muziki wa dansi, JB Mpiana kutoka Congo, na kupata mashabiki kiduchu huku umeme ukizingua katika viwanja vya Leaders na Jenereta kugoma kuwaka, jambo lililopelekea Mkurugnezi wa Bendi hiyo, Mama Sakina, kuanguka na kupoteza fahamu na kukimbizwa Hospitalini.
 Wanenguaji wa Bendi ya Mashujaa, wakishambulia mbele ya mashabiki wao wakati wa uzinduzi huo.
 Rais wa Fm Academia, Nyoshi (kushoto) akiwangoza wanenguaji wake kushambulia jukwaa wakati wa uzunduzi huo kwa staili zao 350 walizozitambulisha kati 700.

No comments:

Post a Comment