Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akipokea cheti maalum cha ulezi wa heshima wa Chama cha wenza wa mabalozi wa nchi za Afrika walioko nchini Ubelgiji (Honory Patronese of the Association of the Spouses of African Ambassadors in Belgium) kutoka kwa Mke wa Balozi wa Cameroon nchini Ubelgiji Mama Christiane Eloundov de Evina wakati wa chakula cha mchana walichowaandalia wake wa Marais wa Afrika jijini Brussels tarehe 2.4.2014
Mke wa Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji Mama Adelaida Kamala akimkabidhi Cheti Maalum cha ulezi wa heshima cha wenza wa mabalozi wa Afrika walioko Ubelgiji, Mke wa Rais wa Cameroon Mama Chantal Biya wakati wa chakula cha mchana walichowaandalia wageni hao kwenye hoteli ya Sheraton.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wake wa Marais na Wakuu wa nchi za Afrika pamoja wa wenza wa Mabalozi wa nchi hizo mara baada ya kupata chakula cha mchana kilichoandaliwa na wenza hao
************************************
Na Anna Nkinda – Brussels, Ubelgiji
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete amepewa cheti na Umoja wa wake wa Mabalozi wa Afrika waishio katika nchi za Jumuia ya Ulaya kwa kutambua na kuthamini mchango wake na kazi anazozifanya za kuwasaidia wanawake, wasichana na watoto wa Tanzania.
Cheti hicho amekabidhiwa jana katika hafla fupi ya chakula cha mchana kilichoandaliwa na wake hao wa mabalozi katika ukumbi wa mikutano uliopo Hoteli ya Sheraton mjini Brussels.
Mama Kikwete ni mmoja kati ya wake wa Marais wa tano wa Afrika waliokabidhiwa vyeti hivyo vya heshima kutokana na kazi zao wanazozifanya za kuisaidia jamii na kuhakikisha kuwa inapata mahitaji ya muhimu kama huduma ya afya na elimu.
Akiongea kabla ya kuwakabidhi wake hao wa marais vyeti hivyo Mke wa Balozi wa Equatorial Guinea ambaye pia ni rais wa umoja huo Mama Mangue de Nvono Nca alisema nia ya kuanzishwa kwa umoja wao ni kulitambulisha bara la Afrika ambalo linajulikana kuwa na changamoto za njaa, magonjwa, kutokuwa na haki na usalama wa kutosha katika nchi za Ulaya.
No comments:
Post a Comment