Tuesday, June 25, 2013

*TANZANIA YASHINDA TUZO 3 ZA UTUMISHI WA UMMA BARANI AFRIKA NCHINI GHANA.


 By Pascal Mayalla  
Tanzania imeshinda tuzo tatu za juu za ubunifu katika Utumishi wa Umma, barani Afrika, kufuatia Tasisi tatu za Tanzania, kushinda nafasi ya kwanza, na kukabidhiwa vikombe vya ushindi na rais wa Ghana, wakati wa kilele cha maadhimisho ya Siku ya Utumishi wa Umma barani Afrika, yaliyofanyika jana mjini Accra nchini Ghana.

Taasisi za Tanzania zilizoshinda ni Ofisi ya  Ukaguzi ya Taifa, (NAO), Wakala wa Vipimo, (WMA),  na Wakala wa Vitambulisho vya Taifa, (NIDA) kufuatia kufanya vizuri katika maonyesho ya  siku 7 ya shughuli mbalimbali za utumishi wa umma yaliyofikia kilele tarehe 23/06/2013.

Akiuzungumzia ushindi huo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Mhe. Celina Kombani, amezipongeza taasisi hizo, zilizolitea sifa taifa hili na kuelezea kufarijika kwake na ushiriki wa  mkubwa wa Tasisi za Tanzania katika maonyesho hayo ambapo jumla ya taasisi 42 kutoka Tanzania, zilishiri.

Akisoma hotuba katika kilele cha maandimisho hayo, Mhe. Kombani ambaye pia ni Mwenyekiti wa Mawaziri wa Utumishi Barani Afrika, amewataka watumishi wa umma kote barani Afrika, kuwatumikia wananchi kwa  bidii,
unyenyekevu, uadilifu wa hali ya juu, na kueleza utumishi wa umma ni kuwatumikia watu.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Gearge Yambesi, amekiri kuwa Tanzania ni moja ya nchi zinazofanya vizuri sana katika utumishi wa umma barani Afrika, hali inayofanya Tanzania kujijengea heshima kubwa barani Afrika na Ulimwenguni kwa ujumla.

Wakizungumzia kuhusu ushiriki wa Tanzania katika maonyesho hayo, Waziri , Mhe. Celina Kombani,  na Katibu Mkuu, Bwana. George Yambesi, wanaeleza zaidi.


Akizungumzia maonyesho hayo, Mkurugenzi wa Kampuni ya Press and Public Relations (PPR), Bw. Pascal Mayualla, amesema mfulululizo wa vipindi vya redio na Televisheni, kuhusu ushiriki wa Tanzania, katika Maonyesho ya Utumishi wa Umma barani Afrika, vitaanza kuonekane kesho, katika vituo mbalimbali vya redio na Televisheni.

No comments:

Post a Comment