Tuesday, June 25, 2013

*WANASWA KWENYE BODABODA WAKIWA NA BASTOLA YENYE RISASI NJE YA BENKI YA POSTA DAR


 Askari kanzu (kulia) akiwa ameshika bastola aliyokutwa nayo mtu mmoja aliyekuwa amepakiwa katika pikipiki aina ya Boxer yenye namba za usaji T 961 CJW katika mtaa wa Makunganya jirani kabisa na benki ya Posta jijini Dar es Salaam leo mchana. Kutokana na kuongezeka kwa matukio ya ujambazi wa kutumia pikipiki na silaha, polisi wameimarisha ulinzi na hasa katika maeneo ya mabenki, ambapo leo wamebahatika kucheza karata yao ya kwanza na kuwanasa jama hao. Haikuweza kufahamika mara moja kuwa jamaa hao waliokutwa na silaha hiyo kuwa walikuwa wakiimiliki kihalali ama la, na sababu za kuwa eneo hilo mida hiyo ya mchana wakiwa na silaha hiyo.
 Watuhumiwa hao wakijaribu kuwasiliana na ndugu jamaa zao kutafita msaada, baada ya kunaswa.
Askari Kanzu, akiikagua silaha hiyo na kukuta ikiwa na risasi za kutosha......Picha kwa hisani ya Habari Mseto Blog

No comments:

Post a Comment