Monday, June 10, 2013

*TAIFA STARS YAREJEA DAR KUANZA KAMBI YA KUWAKABILI KINA DROGBA


Baadhi ya Wachezaji wa timu ya Taifa 'Taifa Stars' wakiwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere leo asubuhi wakitokea Marrakech Morocco, baada ya kumaliza mechi yao ya marudiano na Morocco, mchezo wa kufuzu kombe la dunia Brazil 2014 uliochezwa juzi usiku uliomalizika kwa Stars kufungwa mabao 2-1. Wachezaji hao baada ya kuwasili wanaelekea kuanza tena kambi katika Hoteli ya Tansoma jijini Dar es Salaam kwa ajili ya maandalizi natoka Uwanja wa Ndege  na kuelekea kambini  Hotel, kuanza maandalizi ya mchezo ujao dhidi ya Ivory Coast unaotarajia kupigwa mwishoni mwa wiki hii kwenye Uwanja wa Taifa jijini.

No comments:

Post a Comment