Tuesday, June 10, 2014

MHE. WAZIRI WA NISHATI NA MADINI PROF SOSPETER MUHONGO NA UJUMBE WAKE WATEMBELEA UBALOZI WA TANZANIA WASHINGTON DC

 Mhe. Waziri wa Nishati na Madini Prof Sospeter Muhongo akiongea machache na kumshukuru Mhe. Balozi Liberata Mulamula kwa makaribisho mazuri na kuelezea sababu ya ujio wake nchini Marekani ambao alianzia New York kwenye mkutano wa  mwongo wa Nishati Endelevu kwa wote (SE4ALL) ambao Katibu  Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban   Ki Moon,  siku ya alhamisi wiki iliyopita aliuzindua rasmi   mkutano  uliohudhuriwa na  wajumbe zaidi wa  1,000 wakiwamo zaidi ya mawaziri 20 wa Nishati, wafanyabishara,  mashirika ya kimataifa yakiwamo ya fedha na  Asasi zisizokuwa za kiserikali,
Ujumbe wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Mkutano huu ambao  ulianza  Juni 4 na kumalizikaJuni 6, uliongozwa na  Waziri wa  Nishani na Madini Professor   Sospeter Muhongo ambaye  pamoja na  kuhudhuria  na kuchangia mijadala mbalimbali,    ijumaa ( June 6),  alizungumza katika mkutano wa mawaziri kuhusu  nafasi ya Nishati katika  Ajenda  za Maendeleo Endelevu baada  ya 2015 na  utayari wa Tanzania kuwa mwenyeji wa mkutano wa Bara la Afrika kuhushu Nishati Endelevu kwa wote unaotarajiwa kufanyika mapema mwakani.

No comments:

Post a Comment